RAZA LEE AWAPA TAFU MABINGWA WATETEZI WA ROLLING STONE

Mwana michezo Mohd Ibrahim “Raza Lee” ambae ni mtoto wa Mbunge wa Jimbo la Kiemba Samaki Ibrahim Raza asubuhi ya leo ameisaidia mipira timu ya kombain ya Mjini Unguja ambao ni Mabingwa  watetezi wa Mashindano ya Vijana ya Rolling Stone, Mashindano ambayo yanatarajiwa kuanza rasmi June 29, 2017 na kumalizika July 9, 2017 jijini Arusha.


Mipira hiyo Raza Lee ameikabidhi timu hiyo Dukani kwake ambalo ni Duka la Vifaa vya Michezo ambapo Ali Othman “Kibichwa” Meneja wa Timu hiyo pamoja na Mohammed Seif “King” kocha wa timu hiyo ndio waliyopokea Mipira hiyo.
Mohd Ibrahim "Raza Lee" akiwakabidhi Mipira Ali Othman "Kibichwa" Meneja na Mohammed Seif "King" Kocha

Comments

Popular posts from this blog

HUYU NDIYE MCHEZAJI MWENYE REKODI YA KUFUNGA MAGOLI MENGI KWENYE MECHI YA TAIFA DHIDI YA BOYS