JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE

Timu za JKU Academy zinaondoka usiku wa leo kwa boti ya usiku kwenda Jijini Dar es salam kisha saa 12 za asubuhi kesho Jumatatu kuanza safari ya Arusha ambapo wanakwenda katika Mashindano ya Vijana ya Afrika Mashariki na Kati (Rolling Stone) mashindano ambayo yanatarajiwa kuanza rasmi July 9-19, 2017.

JKU mwaka huu wanatarajia kushiriki timu tatu tofauti katika Mashindano hayo ikiwemo timu chini ya miaka 13, 15 na 17 ambapo msafara wa watu 60 ukitarajiwa kuondoka Visiwani Zanzibar usiku wa leo.

Msafara huo ambao utajumuisha timu tatu tofauti za JKU Academy pamoja na waamuzi wao vijana watano na viongozi watano.

Mashindano ya Rolling Stone mwaka huu yanatarajiwa kuanza rasmi July 9 na kumalizika July 19, 2017 ambapo msimu huu kumepangwa vituo tofauti makundi mengine yamepangiwa Arusha, mengine Manyara.


Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

KMKM KUANDAA MASHINDANO YA RIADHA