Posts

Showing posts from January, 2018

MZEE ZAM WA ZANZIBAR APEWA FUPA NA CAF

Image
Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF), limemteua Mzee Zam Ali kutoka Zanzibar kuwa Kamishna wa mchezo nambari 50 wa kombe la shirikisho kati ya FC Platinum ya Zimbabwe dhidi ya Club Desportivo 1 de Agosto ya Angola mchezo utakaopigwa 20 au 21 ya February, 2018 huko Zimbabwe. Mzee Zam atawasimamia Waamuzi wa Afrika ya Kusini watakaochezesha mchezo huo akiwemo muamuzi wa kati Christopher Harrison, akisaidiwa na muamuzi namba moja Sandile Dilikane na muamuzi namba mbili Thembisile Theophilus huku Muamuzi wa akiba akiwa Tinyiko Victor Hlungwani. “Nimefurahi CAF kuendelea kuwa na imani na mimi kwani wananijua vyema hasa hivi karibuni nilikuwa Kamishna katika Mashindano ya CECAFA Senior Challenge Cup yaliofanyika nchini Kenya, mimi ni mzoefu kuchaguliwa kwenye shughuli za soka kama hizi katika Mashindano mbali mbali”. Alisema Mzee Zam.

UCHAGUZI WA ZAHA UMEWIVA, FEBRUARY 18

Image
Chama cha Mpira wa mikono Zanzibar (ZAHA) kitafanya Uchaguzi wake ambao unatarajiwa kufanyika February 18, 2018. Akizugumza na Mtandao huu Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi Said Ali Mansabu amewataka wadau mbali mbali wa michezo kujitokeza kwa wingi kuchukua fomu kugombea nafasi tofauti kwenye chama hicho. Amesema baadhi ya wadau wanapenda kuwalaumu vingozi hivyo hiyo ni fursa kwao kuja kugombea nafasi katika chama chama hicho. “Mimi nawaomba wanamichezo wenzangu hasa wale wanoumwa na Handa ball, wajitokeze kwa wingi kuchukua fomu katika chama hichi ili kupunguza yale malalamiko ambayo watu wanasema viongozi wana matatizo wa chama hichi basi hii ni fursa ya kupata viongozi wapya”. Alisema Mansabu. Viongozi wapya watakaopatikana katika uchaguzi huo watakaa madarakani kuanzia mwaka 2018 hadi 2022.

LIGI KUU ZENJ SI MCHEZO, TIMU ZINAPIGANA KUTOSHUKA DARAJA

Image

KESHO FAINALI MBILI ZA MAPINDUZI CUP KUPIGWA KATIKA UWANJA WA AMAAN

Image
Fainali ya 12 ya michuano ya Kombe la Mapinduzi Cup inatarajiwa kupigwa kesho kwenye dimba la Amaan kati ya mabingwa watetezi Azam fc kutoka Tanzania bara dhidi ya URA kutokea Uganda, mchezo ambao utapigwa majira ya saa 2:15 za usiku. Bingwa wa Mashindano hayo atazawadiwa Kombe, Shilingi Milioni 10 na Medali za dhahabu wakati mshindi wa pili atapata Milioni 5 na medali za fedha. Wakati huo huo pia kesho kutachezwa Fainali ya ZBC watoto mapinduzi cup mchezo utapigwa majira ya saa 10:30 za jioni kati ya Wilaya ya Mjini dhidi ya Mkoani katika uwanja wa Amaan. Mapema kesho saa 8:00 za mchana uwanjani hapo utachezwa mchezo wa kusaka mshindi wa tatu kati ya Wilaya ya Chake cheke dhidi ya Wilaya ya Kati. Bingwa wa Mashindano hayo atazawadiwa Fedha Taslim shilingi milioni 1, seti moja ya jezi, Kombe kubwa na Medali za dhahabu wakati mshindi wa pili atazawadiwa shilingi laki 7, seti moja ya jezi, kombe na medali za fedha huku mshindi wa tatu atapata shilingi laki 3, kombe dogo, set

SIMBA YAAGA RASMI KOMBE LA MAPINDUZI, SASA YAUNGANA NA TIMU 6 ZA ZANZIBAR KWENDELEA NA KAZI NYENGINE

Image
Timu ya Simba Sports Club imetolewa rasmi katika Mashindano ya Kombe la Mapinduzi baada ya jioni ya leo kufungwa bao 1-0 na URA kwenye mchezo uliopigwa kwenye uwanja wa Amaan. Mchezo huo ulikuwa na kasi huku Simba ikihitaji ushindi ili iingie nusu fainali wakati URA walihitaji japo sare ambapo mpaka dakika 90 kumalizika Simba akikubali kulala mbele ya Waganda hao wa URA. Bao pekee la URA limefungwa na Kalama Deboss dakika 45. Mara baada ya kumalizika mchezo huo kocha wa Simba Masoud Djuma amekiri kuwa Mashindano magumu lakini wamejifunza mengi licha ya kutolewa na sasa wanajiandaa kufanya vyema kwenye ligi kuu soka Tanzania bara. Nae Paulo Okata kocha wa URA amesema sasa kikosi chake kinazidi kuimarika kila siku huku akiwa hana wasi wasi kukutana na timu yoyote kwwenye nusu fainali kati ya Singida United au Yanga. Katika Kundi hilo A timu URA imeongoza ikimaliza na alama 10, huku Azam ikishika nafasi ya pili kwa points zake 9 na sasa URA anasubiri mshindi wa pili wa

BALOZI SEIF AWEKA JIWE LA MSINGI UWANJA WA MAO TSI TUNG

Image
Na Othman Khamis Ame Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alisema ujenzi wa Viwanja vya Michezo Nchini uliomo ndani ya Programu ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar unaudhihirishia Ulimwengu azma ya Zanzibar ya kutaka kukuza sekta ya Michezo Nchini ili irejee katika hadhi yake Kimataifa. Amesema Viwanja hivyo vitakapokamilika vitaweza kusaidia uzalishaji wa Wanamichezo bora watakaoiweka Zanzibar katika Ramani ya Dunia kimichezo kama walivyofanya Zanzibar Heroes na Wanakabumbu wa Soka la Ufukweni Zanzibar Beach Sand Heroes. Balozi Seif Ali Iddi amesema hayo wakati akiweka jiwe la msingi la Ujenzi wa uwanja wa Michezo wa Mau Tse Tung ikiwa ni muendelezo wa harakati za shamra shamra za sherehe za maadhimisho ya kutimia Miaka 54 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ya Mwaka 1964. Alieleza kwamba ujenzi wa Uwanja wa Mau Tse Tung ni jitihada kubwa zinazochukuliwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dr. Ali Mohamed Shein katika kuende