Posts

Showing posts from July, 2018

LIGI KUU YA ZANZIBAR KUENDELEA TENA KESHO KAMA KAWAIDA

Image
Mzunguko wa pili wa ligi kuu soka ya Zanzibar hatua ya nane bora inatarajiwa kuanza kesho Jumamosi kwa kuchezwa michezo miwili katika viwanja viwili tofauti. Katika uwanja wa Amaan majira ya saa 10:00 za jioni watacheza kati ya timu ya Mafunzo dhidi ya Zimamoto ambapo muda huo huo katika uwanja wa Gombani kisiwani Pemba Mwenge watakuwa na kazi kucheza na wanajeshi timu ya Hardrock. Katika michezo ya mzunguko wa kwanza Jamhuri walitoka sare ya 0-0 na Mwenge huku JKU nao wakavutana na Zimamoto kwa kwenda sare ya 2-2 ambapo KVZ walianza na ushindi baada ya kuwafunga Mafunzo mabao 2-1 huku Hardrock nao walianza vyema baada ya kushinda bao 1-0 dhidi ya Opec.

KAMATI TENDAJI YA ZFA YAVUNJWA, WENGINE WAPYA KUCHUKUA NAFASI

Image
Mrajisi wa vyama vya michezo Zanzibar ameufungia uongozi wa kamati tendaji ya ZFA ambao upo kwa mujibu katiba ya ZFA ya mwaka 2010 kwa kushindwa kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa katiba yao. Akizugumza na wandishi wa habari ukumbi wa uwanja wa Amani mjini Unguja Sleman Pandu Kweleza amesema ofisi ya mrajisi wa vyama vya michezo Zanzibar imefanya hivyo kwa mujibu wa sheria kwa kuwa ndio wanao simamia vyama vya michezo vyote Zanzibar. Akitoa sababu ya kufungia kamati hiyo mrajisi Pandu Kweleza amesema baada ya kushindwa na kuupuza ombi la mrajisi la kutaka badhi ya vifungu vya katiba yao ya ZFA kufanya marekebisho na kushindwa kufanya hivyo, aidha mrajisi amefafanua alindakia barua kamati tendaji ya ZFA tarehe 20/3/2018 yenye kumbu kumbu no BTMZ /MRJS/ VOLUME/10 ya kutaka kufanya marekibisho baadhi ya maeneo ya katiba ya ZFA. Aidha kwa upande mwengine mrajisi amesema kamati tendaji ya ZFA imeshindwa kusimamia kanuni za michezo na kusababisha ligi kuu ya Zanzibar kuonekana

LIGI KUU ZANZIBAR MSIMU WA MWAKA 2017-2018 KUENDELEA TENA KESHO

Image
Ligi kuu soka ya Zanzibar hatua ya nane bora msimu wa mwaka 2017-2018 inatarajiwa kuanza rasmi kesho kwa kupigwa michezo miwili katika Viwanja viwili tofauti majira ya saa 10:00 za jioni. Katika uwanja wa Amaan wataanza kucheza timu ya JKU dhidi ya Zimamoto ambapo katika uwanja wa Gombani Kisiwani Pemba Mwenge wataivaa timu ya Jamhuri. Hatua hiyo ndio itakayotoa Bingwa na Makamo Bingwa wa Zanzibar watakaowakilisha Zanzibar katika Mashindano ya Klabu Bingwa na Kombe la Shirikisho Barani Afrika ambapo timu nne za Unguja zilizofanikiwa kutinga hapo ni JKU (Mabingwa Watetezi), Zimamoto (Makamo Bingwa), Mafunzo na KVZ huku kwa upande wa Kanda ya Pemba ni Jamhuri, Mwenge Opec na Hardrock.

KOCHA KING ATANGAZA WACHEZAJI 20 WATAKAOKWENDA ARUSHA ROLLING STONE

Image
Kocha mkuu wa Timu ya Kombaini ya wilaya ya mjini Muhamed Seif King ametangaza majina ya wachezaji ishirini watakaounda kikosi hicho kinacho tarajia kuelekea  kwenye mashindano ya Rolling Stone Mkoani Arusha Mwezi huu. Akikitangaza kikosi hicho kinacho husisha wachezaji wenye umri wa miaka 13 hadi 17 kwa mujibu wa kanuni ya mashindano hayo Kocha King amewatangaza Walinda Mlango Mwinyi Ali, Ahmada Abdulrahman. Kwa upande wa Walinzi Abdallah Saidi, Abdulahamid Ramadhan, Mudathir Nassor, Mussa Mohamed, Mohamed Haji, Khalid Khamis,Makame Mohamed na Abubakar Suleiman. Kwa upande wa Viungo wameitwa Yahaya Silima, Fahad Mussa, Kassim Suleiman, Mustapha Muhsin, Yassir Ali, Ibrahim Ali   na Mohamed Khamis. Kwa upande wa washambuliaji ni Ibrahim  Yahya , Nassor Saleh, Yussufu Bwanga, Muhamed Daudi na Yussufu Saidi Jussa. Aidha Kocha Seif King amesema kikosi hicho kinaendelea na mazoezi uwanja wa Amani na kinaendelea kujipima mechi za kirafiki na vilabu mbali mbali . Kombaini ya wi