Posts

Showing posts from September, 2017

TIMU YA TAIFA YA ZANZIBAR YA MPIRA WA MEZA YASHINDANA NA KAKA ZAO WA BARA KUTAFUTA TIMU YA TANZANIA ITAKAYOKWENDA AUSTRALIA

Image
Mashindano maalum ya mchujo wa kutafuta timu ya Taifa ya Mpira wa Meza Tanzania yameanza leo na kumalizika kesho Jumapili kwenye Ukumbi wa Shule ya Msingi Kisutu Jijini Dar es salam. Katika mchujo huo timu ya Taifa ya Zanzibar inachuana na wenzao wa Tanzania bara kwaajili ya kupata wachezaji wawili watakaowakilisha Tanzania katika Mashindano ya Jumuiya ya Madola ambayo yatafanyika Gold Coast Australia kuanzia April 4-15, 2018. Jumla ya Wachezaji 10 wanagombania nafasi hizo 2 za kwenda Australia ambapo Wachezaji kutoka Zanzibar wapo wawili ambao ni Mohammed Shaabani na Khalid Ahmed. Wachezaji hao 10 watacheza kwa mizunguko 9 ambapo kila mmoja atacheza na mwenzake na wawili wa mwanzo ndio watakaofanikiwa kwenda huko Australia. Zaidi endelea kufatilia Blog hii kupata taarifa kwa kina kwenye kinyanganyiro hicho.

MATOKEO YA WILAYA YA KUSINI

Na Abdulhamid Ali,  Kusini Unguja. MATOKEO LIGI DARAJA LA PILI WILAYA YA KUSINI LEO. KWENYE UWANJA WA SUNGUSUNGU,  MBUYUNI 1 - 1 KIBUTENI. GOLI LA KIBUTENI LIMEFUNGWA NA IDDI HAJI KWENYE DAKIKA YA 26 NA LA MBUYUNI  ABDALLAH MSELEM  KWENYE DAKIKA YA 77. KWENYE UWANJA WA MUUNGONI, PAJE STAR 3 - 1 PETE STAR. KWENYE UWANJA WA JAMHURI,  UHURU 1 - 1 GEREJI. KESHO KWENYE UWANJA WA SUNGUSUNGU NAIROGWE WATACHEZA NA NEW BOYS. AZIMIO NA DULLA BOYS KWENYE UWANJA WA JAMHURI NA NYOTA NYEUSI WATACHEZA NA NEW GENERATION KWENYE UWANJA WA  MUUNGONI.

TAIFA JANG’OMBE NA KWEREKWE CITY HAPATOSHI HAPO

Image
Wachezaji wa Taifa ya Jang'ombe  Timu ya Taifa ya Jang’ombe (Wakombozi wa Ngambo) ambao wanashiriki ligi kuu soka ya Zanzibar, wanatarajia kucheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Kwerekwe City inayoshiriki ligi daraja la Pili Taifa Unguja. Mchezo huo utapigwa siku ya Jumapili ya Oktoba 1, 2017 saa 1:00 za usiku katika uwanja wa Amaan. Mechi yao ya kwanza ya ligi kuu soka ya Taifa ya Jang’ombe itacheza dhidi ya  Zimamoto mchezo ambao utapigwa Oktoba 5 mwaka huu saa 8:00 za mchana katika uwanja wa Amaan.   Benchi la Ufundi la Kwerekwe City

MATOKEO YA LIGI DARAJA LA PILI WILAYA YA MJINI HAYA HAPA

MATOKEO LIGI DARAJA LA PILI WILAYA YA KUSINI ILIYOANZA LEO JUMATANO Na Abdulhamid Ali, Kusini Unguja. MAPEMBE 1- 0 SIMBA WA NYIKA. Uwanja wa Sungusungu. ALBINO 1 - 2 SHUKRAN.Uwanja wa Beach boys. Fc BOTAL 2 - 1 DIMBANI. Uwanja wa Jamhuri. KESHO ALHAMIS. Mapinduzi v Jozani. Sungusungu. Alhapa v Nyota nyeupe. Jamhuri. Beach boys v Mashambulizi. Uwanja wa Beach boys Muungoni.

TAIFA YA JANGOMBE YAREJEA ZANZIBAR WAKITOKEA KAMBI TANGA

Image
Timu ya Taifa ya Jang’ombe wamerejea Visiwani Zanzibar jioni ya leo wakitokea mkoani Tanga ambapo waliweka kambi ya wiki mbili. Mara baada ya kuwasili tu Unguja Taifa wakaenda kumjulia hali mdhamini wao mkuu Salim Hassan Turkey huko Mpendae Mjini Unguja. Turkey ambae pia ni mbunge wa Jimbo la Mpendae amefurahishwa mno kutembelewa na vijana wake ambapo pia amesema wakitwaa ubingwa wa ligi kuu soka ya Zanzibar msimu huu atawafanyia jambo kubwa wachezaji hao. “Nawapongeza kwa kuja kunijuulia hali, ahsanteni wachezaji wangu, mwaka jana niliahidi mukichukua ubingwa ntakupelekeni China kukaa kambi, lakini kwa bahati mbaya hatukuchukua ubingwa ndo mana tukaenda kambi Tanzania bara, lakini msimu huu ntaangalia mechi mbili kasha ntakupeni ahadi nzito”. Alisema Turkey. Wakati huo huo kocha mkuu wa Taifa ya Jang’ombe Saleh Juma Maisara amesema kambi yao ilikuwa nzuri sana na imewasaidia kujijenga vizuri zaidi kwenye ligi kuu ambapo kwasasa kikosi chake kipo tayari kupamba

THEO KOMBAIN YATOLEWA KATIKA MASHINDANO YA NDONDO CUP NA KIBONDE MAJI

Image
Matokeo ya leo Jumapili 24/9/2017 nusu fainali ya kwanza. Dakika 90, Theo Kombain 1-1 Kibonde Maji , Penalty Kibonde maji 4-3 Theo. KESHO Jumatatu 25/9/2017 Six center vs Amazon fc katika uwanja wa blue star Mwera saa 10: 00 za jioni. Mashindano hayo ya Ndondo CUP awali yalianza na timu 63 kwa kuchezwa mtoano na mpaka sasa kufikia hatua ya nusu fainali  ambapo bingwa anatarajiwa kupatiwa Ng'ombe na Shilingi Milioni moja. Mashabiki wa Kibonde Maji wakishangiria ushindi

TEDDY: WAAMUZI ZANZIBAR WATALIPWA KABISA KABLA YA KAZI

Image
Waamuzi watakaochezesha Mashindano yanayosimamiwa na ZFA Taifa wameahidiwa kulipwa pesa zao kabisa kabla ya kuanza kwa ligi ili kuepusha kutowajibika kikamilifu. Ameyathibitisha Katibu Mkuu wa Chama cha Soka Visiwani Zanzibar Mohammed Ali Hilali (Teddy) ambapo amesema msimu huu watawalipa waamuzi kabisa kabla ya kuanza kwa ligi ili wazidi kusimamia vyema sheria 17 za soka. “Nahakikisha baada ya siku nne kutoka leo (Jana) pesa za Waamuzi zote za msimu huu ntamkabidhi Mwenyekiti wa kamati ya Waamuzi, hatutaki kudaiwa tena msimu huu, tutawapa chao kabisa ili tuwadai wao mechi na si kutudai sisi". Alisema Teddy. Ligi kuu soka visiwani Zanzibar inatarajiwa kuanza Jumanne ya Oktoba 3, mwaka huu ambapo mechi za awali ni Mafunzo Vs JKU saa 8:00 mchana kisha Jang'ombe Boys Vs KMKM saa 10:00 jioni katika uwanja wa Amaan.

WAAMUZI WA ZANZIBAR WALIOFAULU KOPA TEST HAWA HAPA

Image
Kamati ya Waamuzi Visiwani Zanzibar imetangaza majina ya Waamuzi waliofaulu katika mtihani wa utimamu wa mwili (Kopa Test) uliofanyika juzi Amani Mjini Unguja. Akizungumza na Mtandao huu katibu wa Kamati ya Waamuzi Zanzibar Muhsin Ali "Kamara" amesema jumla ya Waamuzi 56 walifanya mtihani huo  ambapo Waamuzi 34 ndio waliyofaulu huku Waamuzi 22 walifeli. Kamara amewataja Waamuzi hao 34 waliofaulu ni Omar Abdallah Khamis, Kassim Suleiman Sereji, Mohammed Khamis Mwadin, Mohammed Ali Mohammed, Nassor Salum Masoud, Ali Ramadhan Rajab (Kibo mdogo), Nassir Salum Sihai (Msomali), Abeid Juma Khamis na Iddi Khamis Mberwa. Wengine ni Mariam Chalse Mattius, Ruwaida Abdallah Khamis, Mwanahija Foum Makame, Dalila Jaffar Mtwana, Mgaza Ali Kinduli, Mbaraka Haule Haule, Mfaume Ali Nassor, Rashid Farahan Issa (Webb), Mohammed Kassim Mohammed, Mohammed Omar Haji, Omar Bakar Omar, Mohammed Rajab Mgeni, Mustafa Abdallah Khamis, Sharifu Haji Mohammed, Issa Haji Vuai, Ramadhan Keis Ramadhan

RATIBA YA NUSU FAINALI COCO SPORTS NDONDO CUP , BINGWA MTETEZI THEO KOMBAIN WATAKIPIGA NA KIBONDE MAJI

Image
Kamati inayosimamia Mashindano ya Coco Sports Ndondo Cup leo imetangaza ratiba ya nusu fainali ya mwaka 2017. Hii ndio nusu fainali ya COCO SPORTS NDONDO CUP 2017 Jumapili 24/9/2017 Theo Kombain vs Kibonde Maji Jumatatu 25/9/2017 Six center vs Amazon fc Mechi zote zitapigwa katika uwanja wa blue star Mwera saa 10: 00 za jioni. Mashindano hayo ya Ndondo CUP awali yalianza na timu 63 kwa kuchezwa mtoano na mpaka sasa kufikia hatua ya nusu fainali   ambapo bingwa anatarajiwa kupatiwa Ng'ombe na Shilingi Milioni moja.

SHANGANI NA MUEMBE MAKUMBI ZANGARA WILAYA YA MJINI

Image
Timu ya Shangani na Muembe Makumbi zimeanza vyema ligi daraja la Pili Wilaya ya Mjini baada ya kushinda michezo yao ya leo kwenye uwanja wa Amaan. Saa 10 za jioni Shangani waliichapa Gereji 2-0 kwa mabao yaliyofungwa na Abdallah Maulid dakika ya 42 na Pesto Is-haka dakika ya 45. Saa 8 za mchana Muembe Makumbi wakaichapa Kundemba bao 1-0 kwa bao pekee lililofungwa na Ame Ibrahim Mohammed dakika ya 76. Ligi hiyo itaendelea tena kesho kwa kupigwa michezo miwili katika uwanja wa Amaan. Saa 8:00 za mchana El hilali dhidi ya Kijangwani na saa 10:00 za jioni Gulioni City dhidi ya Raskazone. Yahya Juma Ali Katibu wa ZFA Wilaya ya Mjini

GULIONI YAANZA KWA KISHINDO WILAYA YA MJINI

Image
Timu ya Soka ya Gulioni FC imeanza vyema ligi daraja la Pili Wilaya ya Mjini baada ya kuitandika Dira FC mabao 5-0 kwenye mchezo uliopigwa saa 8 za mchana katika uwanja wa Amaan. Mabao ya Gulioni yamefungwa na Maulid Salum Abdallah akipiga Hat trick dakika ya 14, 48 na 88 huku mabao mengine yakifungwa na Haji Juma Ali dakika ya 22 na 24. Ligi hiyo itaendelea tena kesho kwa kupigwa michezo miwili katika uwanja wa Amaan. Saa 8:00 za mchana wataanza Shangani dhidi ya Gereji, na saa 10:00 za jioni watasukumana kati ya Kundemba dhidi ya Muembe Makumbi.