Posts

Showing posts from June, 2019

MKOA WA KUSINI UNGUJA TISHIO TFF CUP U-17

Image
Kikosi cha Mkoa wa Kusini Unguja Timu ya Mkoa wa Kusini Unguja imeendeleza wimbi lake la ushindi baada ya kushinda michezo miwili mfululizo ya mwanzo kufuatia asubuhi ya leo kufanikiwa kuifunga timu ya Mkoa wa Mbeya mabao 2-1 kwenye Mashindano ya TFF ya Vijana chini ya umri wa miaka 17 (U-17) kwenye uwanja wa Mabatini Mlandizi. Katika mchezo huo timu ya Mbeya ilitangulia kupata bao dakika ya 43 kipindi cha kwanza kwa bao la Bernard Peter lakini Kusini wakajipanga upya kipindi cha pili kwa kusawazisha na kuongeza bao kwenye dakika ya 55 na 70 kwa Mabao Ramadhan Mwita Haji na Hafidh Othman Kombo. Huu ni ushindi wa Pili kwa Mkoa wa Kusini Unguja kufuatia mchezo wa kwanza kuifunga Lindi bao 1-0 ambapo sasa ina alama 6 na kuongoza kundi lao B. Wawakilishi wengine wa Zanzibar kwenye Mashindano hayo timu ya Mkoa wa Mjini Magharibi leo imejikuta ikipoteza baada ya kufungwa na Mkoa wa Songwe mabao 2-1 mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa Kibaha.

JEMBE JENGINE KUTOKA ZANZIBAR RASMI AMETUA YANGA

Image
Timu ya Yanga imemalizana rasmi na Mlinzi wa timu ya KMC, Ally Hamad Ally 'Kinibu' baada ya kusaini mkataba wa miaka miwili. Ally ambae aliwahi kucheza Gulioni FC ya Zanzibar kabla kwenda Stand United na msimu ulopita akiitumikia KMC. Kusajiliwa kwa Ally Ally kunaifanya klabu ya Yanga kuwa na orodha kubwa ya Wachezaji kutokea Visiwani Zanzibar akiwemo kiungo pendwa Feisal Salum (Fei toto), Mohammed Issa (Moo Banka), Abdul Aziz Makame (Abui) na wengine wengi ambao wamemaliza mikataba msimu ulopita .

TIMU ZA ZANZIBAR ZAANZA KUTINGA ROBO FAINALI UMISSETA MTWARA

Image

TIMU ZA UNGUJA UMISSETA UTAZIPENDA TU

Image

ZANZIBAR YASHINDA TENA MTWARA UMISSETA

Image

ZANZIBAR RAHA RAHA TU, UMISSETA MTWARA

Image

ZANZIBAR YAANZA VYEMA, MICHEZO UMISSETA MTWARA

Image

ZANZIBAR IMEWASILI SALAMA MTWARA | kisanduTV #KisanduTV #KisanduHabariMi...

Image

TIMU ZA ZANZIBAR ZIMEAANZA VYEMA MASHINDANO YA UMISSETA

MASHINDANO ya umoja wa michezo kwa skuli za sekondari Tanzania Umisseta, yameanza kutimia vumbi katika viwanja vya Chuo cha Ualimu Ufundi Mkoani Mtwara, huku Zanzibar ikianza kwa kishindo michezo hiyo. Katika Mashindano hayo timu ya mpira wa kikapu ya kanda ya Pemba imetoka na ushindi wa vikapu 36 -15 dhidi ya Singida huku Unguja nayo mpira wa Kikapu imeanza kwa kishindo baada ya kuichapa Kigoma vikapu 38-23. Kwa upande wa mpira wa Wavu timu ya Kanda ya Pemba imetoka na ushindi wa seti 3-1 dhidi ya Mara kwa wanawake na wanaume Pemba ikakubali kichapo cha seti 3-0 dhidi ya Ruvuma ambapo Unguja Wavu ikachapwa na Mbeya kwa seti 3-1. Katika Soka Zanzibar haikuanza vizuri baada ya Unguja kutoka sare ya 0-0 dhidi ya Dodoma huku Pemba wakichapwa 3-1 na Katavi ambapo mpira wa Pete Unguja ikifungwa na Dodoma mabao 21-12.

SOKA LA ZANZIBAR LAPATA UONGOZI MPYA, SEIF BOSS ASHINDA UCHAGUZI WA ZFF

Image
Kushoto rais mpya wa ZFF Seif Kombo Pandu, wa kati ni Khamis Abdallah Said na kulia ni Ame Abdallah Dunia walikuwa wagombea Urais ZFA Kilio cha wadau wa soka wa Zanzibar cha kutaka kufanyika uchaguzi mkuu ndani ya shirikisho la mpira wa miguu Zanzibar kimemalizika baada ya kamati ya uchaguzi  iliopewa jukumu kukamilisha zoezi hilo. Uchaguzi huo ambao umefanyika leo katika ukumbi wa makao makuu ya chuo cha Mafunzo Kilimani mjini Unguja, wajumbe wa mkutano mkuu wamemchagua Seif Kombo Pandu kuwa rais wa shirikisho hilo kwa  mara ya kwanza baada ya kupata asilimia 57 ya kura zilizopigwa kwa kujikusanyia kura 16 kati ya kura 28. Baadhi ya Wajumbe wa Mkutano Mkuu kwenye uchaguzi wa ZFF Kiti hicho cha urais ambacho kiligombaniwa na wajumbe watatu ambapo Seif Kombo  amechukuwa urais huwo baada ya kuwapita wapinzani wake Ame Abdalla Dunia aliepata kura tano na Khamis Said Abdalla aliepata kura 7. Hata hivyo wajumbe hao wamemchagua Salum Ubwa Nassor kuwa makmo wa rais  wa s