SIMBA YAAGA RASMI KOMBE LA MAPINDUZI, SASA YAUNGANA NA TIMU 6 ZA ZANZIBAR KWENDELEA NA KAZI NYENGINE

Timu ya Simba Sports Club imetolewa rasmi katika Mashindano ya Kombe la Mapinduzi baada ya jioni ya leo kufungwa bao 1-0 na URA kwenye mchezo uliopigwa kwenye uwanja wa Amaan.

Mchezo huo ulikuwa na kasi huku Simba ikihitaji ushindi ili iingie nusu fainali wakati URA walihitaji japo sare ambapo mpaka dakika 90 kumalizika Simba akikubali kulala mbele ya Waganda hao wa URA.

Bao pekee la URA limefungwa na Kalama Deboss dakika 45.

Mara baada ya kumalizika mchezo huo kocha wa Simba Masoud Djuma amekiri kuwa Mashindano magumu lakini wamejifunza mengi licha ya kutolewa na sasa wanajiandaa kufanya vyema kwenye ligi kuu soka Tanzania bara.

Nae Paulo Okata kocha wa URA amesema sasa kikosi chake kinazidi kuimarika kila siku huku akiwa hana wasi wasi kukutana na timu yoyote kwwenye nusu fainali kati ya Singida United au Yanga.
Katika Kundi hilo A timu URA imeongoza ikimaliza na alama 10, huku Azam ikishika nafasi ya pili kwa points zake 9 na sasa URA anasubiri mshindi wa pili wa kundi B kati ya Yanga au Singida United ambao kwasasa wanacheza kwenye mchezo wa mwisho wa kundi B ambapo Yanga ana alama 12 sawa sawa na Singida ambao wote wameshatinga nusu fainali kwenye kundi lao B.

Sasa Simba wataungana na timu sita za Zanzibar ambazo zimeshatoka zikiwemo JKU, Zimamoto, Taifa ya Jang’ombe, Mlandege, Mwenge na Jamhuri.
Baadhi ya Waamuzi wanaochezesha kombe la Mapinduzi wakitokea Zanzibar

Comments

Popular posts from this blog

HUYU NDIYE MCHEZAJI MWENYE REKODI YA KUFUNGA MAGOLI MENGI KWENYE MECHI YA TAIFA DHIDI YA BOYS