WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

Kocha mkuu wa timu ya taifa ‘Taifa Stars’ Salum Mayanga ametangaza kikosi cha wachezaji 23 ambao wataingia kambini kwa ajili ya maandalizi ya michezo miwili ya kirafiki ya kimataifa dhidi ya DR Congo na Algeria.

Wachezaji wa tano wa Zanzibar ni mlinda mlango Abdulrahman Mohamed wa JKU, pamoja na viungo Mudathir Yahaya wa Singida United, Feisal Salum wa JKU, Abdulaziz Makame wa Taifa ya Jang’ombe na  Mohamed Issa wa Mtibwa Sugar. 

Kikosi kamili kilichotangazwa na Mayanga kinajumuisha wachezaji wafuatao: Magolikipa ni Aishi Manula, Abdulrahman Mohamed na Ramadhani Kabwili.

Walinzi: Shomari Kapombe, Hassan Kessy, Gadiel Michael, Kelvin Yondani, Erasto Nyoni na Abdi Banda.

Viungo: Hamisi Abdallah, Mudathir Yahaya, Said Ndemla, Feisal Salum, Abdulaziz Makame, Mohamed Issa, Thomas Ulimwengu, Farid Mussa, Shiza Kichuya, Ibrahim Ajib.

Washambuliaji: Mbwana Samatta, John Bocco, Simon Msuva na Yahaya Zayd.

Mara ya mwisho Mayanga alitaja kikosi cha Stars Oktoba 24, 2017 kwa ajili ya mchezo wa kirafiki dhidi ya Benin, wapo wachezaji ambao wametemwa kwenye kikosi kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kushuka kwa viwango vyao pamoja na majeraha lakini pia kuna wachezaji wapya walioitwa baada ya kufanya vizuri siku za karibuni.

Wachezaji walioitwa kwenye kikosi cha Stars ambao hawakuwepo kwenye kikosi kilichoitwa kwa ajili ya mchezo dhidi ya Benin.

Abdulrahman Mohamed, Shomari Kapombe, Hassan Kessy, Faisal Salum, Abdulaziz Makame, Thomas Ulimwengu, John Bocco, Yahaya Zayd na Said Ndemla.

Wachezaji waliokuwepo kwenye kikosi kilichocheza dhidi ya Benin lakini wameachwa kwenye kikosi kilichotajwa leo kutokana na sababu tofauti.

Peter Manyika, Boniphace Maganga, Nurdin Chona, Dickson Daud, Himid Mao, Mzamiru Yassin, Raphael Daud, Abdul Mohamed, Mbaraka Yusuph, Yohana Mkomola.

Comments

Popular posts from this blog

HUYU NDIYE MCHEZAJI MWENYE REKODI YA KUFUNGA MAGOLI MENGI KWENYE MECHI YA TAIFA DHIDI YA BOYS