TIKETI ZA ZFA ZAZUWA GUMZO ZANZIBAR
Ligi
kuu soka Visiwani Zanzibar kanda ya Unguja imeanza rasmi jana kwa kupigwa
michezo miwili katika uwanja wa Amaan, lakini wapenzi wa Soka wamekijia juu
Chama cha Soka Zanzibar (ZFA) baada ya kuziuza tiketi kwenye michezo hiyo
tiketi ambazo zimeshapita muda wake tangu msimu uliopita.
Mashabiki
hao wa soka walishangazwa kununua tiketi ya mechi kati ya Jang’ombe Boys dhidi
ya KMKM na badala yake wakauziwa tiketi zilizoandikwa mchezo wa Jang’ombe boys
na Taifa ya Jang’ombe mchezo ambao tayari umeshachezwa tangu tarehe 30/07/2017.
Mbali
na hilo tiketi wameuziwa shilingi elfu mbili wakati bei iliyoandikwa kwenye
tiketi hizo ni shilingi elfu moja.
Mtandao
huu umemtafuta mmoja wa kiongozi wa ZFA na kusema kwamba kwa hilo hana ufumbuzi
nalo mpaka wahusika zaidi watowe ufafanuzi.
“Mimi
mambo hayo ya tiketi siyajuwi kwa undani, wapo wahusika wakuu ndo wanaweza
kulitolea ufafanuzi, lakini kwetu Zanzibar mbona naona jambo la kawaida mno si
la kushangaza”. Alisema.
modenFmonsyu Gary High https://wakelet.com/wake/wF07J-r-eCVgTtWG6tpY2
ReplyDeletecarsingwhisfi
demoquae-biYonkers Jessica Wright Driver Genius
ReplyDeleteAdobe Media Encoder
Movavi Video Converter
workpulinthumb
inefra-ge Paul Hager Software
ReplyDeletereaislugkannrew