4 BORA KUSAKA TIMU 2 KUPANDA LIGI KUU ZENJ MSIMU UJAO KUANZA LEO

Wachezaji wa Miembeni City


Hatua ya nne bora ligi Daraja la Kwanza Taifa kituo cha Unguja kutafuta timu 2 za kwenda ligi kuu Zanzibar Msimu ujao inatarajiwa kupigwa Leo Jumatatu April 17 michezo miwili katika Uwanja wa Amaan.

Saa 10:00 za Jioni Ngome waatanza kazi kucheza na Seblen United huku mchezo mwengine kupigwa saa 1:00 za usiku kati ya Miembeni City dhidi ya Charawe.

Michezo mengine itapigwa siku ya Jumatano ya  April 26 ambapo saa 10:00 za jioni wataumana kati ya Miembeni City dhidi ya Seblen United, na saa 1:00 za usiku Charawe vs Ngome.

Michezo ya mwisho itapigwa Mei 9, 2017 ambapo saa 10:00 za jioni kumi watasukumana Sebleni United dhidi ya Charawe na saa 1:00 za usiku Miembeni City watamalizana na Ngome michezo yote itachezwa katika uwanja wa Amani mjini Unguja.


Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE