ATTAI NA HUSSEIN WACHINJWA NA ZFA, WAFUNGIWA MAISHA KUTOJIHUSISHA NA SOKA

Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa  ZFA, Mkutano uliofanyika leo Gombani Pemba



Mkutano Mkuu wa dharura wa Chama cha Soka Visiwani Zanzibar “ZFA” umewafukuza wajumbe wake wawili Hussen Ali Ahmada na Massoud Attai na kuwafungia maisha kutojihusisha na Soka kutokana na sababu tofauti.

Maamuzi hayo yameamuliwa katika Mkutano huo wa dharura uliofanyika asubuhi ya leo katika Ukumbi wa Uwanja wa Gombani Kisiwani Pemba.

Akizungumza na Mtandao mara baada ya kumalizika Mkutano huo Ali Bakar “Cheupe” ambae ni Afisa habari wa ZFA amesema sababu zilizopelekea kufukuzwa wawili hao ni kukiuka Maadili ya ZFA na ndio mana wamewatimua kwenye chama chao.

“Mkutano Mkuu leo umeamua kuwafungia maisha kutojishughulisha na soka wajumbe wetu wawili Attai na Hussein, sababu kubwa kwa Hussein yeye alitumia vibaya madaraka wakati ule soka lilikuwa linaongozwa na kamati ya muda na yeye ndie aliyekuwa Mwenyekiti wa kamati hiyo, lakini kwa upande wake Attai yeye alifanya ubadhilifu wa Fedha na pia alituhumiwa kuviibia vilabu ambavyo viliingia katika Mashindano ya Kimataifa zikiwemo Polisi, KMKM, Mafunzo na JKU ambapo fedha alipewa yeye na kule CAF hajazipeleka”. Alisema Cheupe.


Attai alikuwa ni mjumbe wa ZFA Wilaya ya Kaskazini “A” kwenda Taifa huku Hussein yeye alikuwa ni Mjumbe ZFA Wilaya ya Mjini kwenda Taifa ambapo kwasasa Wilaya hizo zinatarajia kufanya Uchaguzi kwa haraka huku Wilaya ya Mjini huwenda ikafanya April 30, 2017.

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE