CHANEZA CHAAMINI VILABU VYAKE VITAREJEA NA VIKOMBE KENYA


Chama cha Netball Zanzibar (CHANEZA) kipo mbioni kukamilisha matayarisho ya mwisho ya Safari kwa vilabu vyake ambavyo vinatarajiwa kwenda Nairobi Nchini Kenya kwenye mashindano ya Klabu bingwa ya Afrika Mashariki ya Netball ambayo yanatarajiwa kuanza April 23-30 mwaka 2017.

Akizungumza na Mtandao huu Katibu wa CHANEZA Said Ali Mansabu amesema Mashindano ya msimu huu yatakuwa na ushindani sana lakini kwa upande wao Zanzibar wamejiandaa vyema kurejea na Vikombe ambapo timu 4 za Zanzibar zikitarajiwa kuwakilisha nchi.

“Mashindano magumu msimu huu lakini sisi Zanzibar tunategemea kupeleka timu 4, na pia naamini tutarejea na vikombe”. Alisema Mansabu.

Vilabu vya Zanzibar vitakavyoshiriki Mashindano hayo ni KVZ, Zimamoto na Mafunzo kwa Wanawake wakati kwa Wanaume watawakilisha JKU pekee.


Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE