CHWAKA AONA MWEZI, CHUONI HOI KWA KIPANGA

Timu ya Chwaka Stars imefanikiwa kuonja ladha ya Ushindi baada ya kuifumua Kimbunga mabao 4-0 katika mchezo wa ligi kuu sika ya Zanzibar kanda ya Unguja uliosukumwa katika uwanja wa Amaan  Saa8 za mchana.
Mabao ya Chwaka yamefungwa na Juma Said dakika ya 4, Hafidh Ramadhan dakika ya 5, Ibrahim Sultan dakika ya 26 na Maombi Zabron dakika ya 89.
Mchezo mwengine uliopigwa saa 10 za jioni timu ya Kipanga walifanikiwa kuifunga Chuoni mabao 2-0.
Mabao ya Kipanga yamefungwa na Muughar Ahmada Jihad dakika ya 65 na David Nyerere dakika ya 89.
Kesho ligi hiyo itaendelea tena katika uwanja wa Amaan saa 8 mchana Polisi dhidi ya Mundu na saa 10 za jioni Kilimani City dhidi ya Kijichi.
Kikosi cha Chwaka Stars

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE