KARANI WA ZFA AKATWA MGUU KWA MARADHI YA SUKARI

Viongozi wa ZFA walipokwenda kumuangalia Karani wao katika Hospitali ya Mnazi Mmmoja




Karani wa Chama chama cha Soka Zanzibar (ZFA) Haji Othman  (Babu Haji) amekatwa mguu jana kwa maradhi ya Sukari baada ya kuwa na vidonda mguuni mwake.

Taarifa tulizozipata kutoka kwa Mjumbe mmoja wa ZFA amesema Karani wao huyo bado yupo katika Hospitali Kuu ya Mnazi Mmmoja Mjini Unguja.

Alisema sababu kubwa ya kufanyiwa uperesheni huo ni baada ya kuwa na vidonda  vya mguu huo na kuonekana  vingezidi kumletea matatizo makubwa mwilini mwake ambapo Madaktari wakalazimika kumkata Mguu huo.

“Ni kweli Karani wetu amekatwa mguu na tumuombee dua kwani ndio mitihani yetu ya Maisha, Mungu atamsaidia”. Alisema  mjumbe huyo.

Mwenyezi Mungu atazidi kumsaidia mgonjwa huyo  na kumpa subra  katika kipindi hiki kigumu.


Makamo Urais wa ZFA Unguja Mzee Zam Ali akimliwaza Babu Haji






Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE