KOMBE LA MUUNGANO KUANZA KESHO IJUMAA KWA KUSHIRIKISHA VILABU VYA BARA NA ZANZIBAR

Kikosi cha Mafunzo
Mashindano ya Muungano ya Mchezo wa Mpira wa Kikapu (Basketball) yanatarajiwa kuanza rasmi siku ya kesho Ijumaa ya April 21 na kumalizika Jumatano April 26, 2017 kwenye uwanja wa Gymkhana ambapo Mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa Makamu wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Iddi.


Akizungumza na Mtandao huu katibu wa chama cha Basketball Zanzibar (BAZA) Abdul-rahman  Mohd Hassan amesema wamejiandaa vizuri msimu huu na watahakikisha mashindano hayo yatakuwa bora kuliko miaka iliyopita.

“Mashindano ya mwaka huu tunatarajia kuwa bora zaidi, vilabu vimepania kufanya makubwa msimu huu, mgeni Rasmi atakuwa Balozi Seif”. Alisema Abdul-rahman. 

Kawaida ya Mashindano hayo hujumuisha vilabu vya juu kwenye ligi kuu ya Basketball ya Tanzania bara na vinne vya juu kwenye ligi ya Zanzibar ambapo ufunguzi watacheza Polisi dhidi ya Mbuyuni saa 10:00 za jioni.

Kwa upande wa Wanaume mpaka sasa timu zilizothibitisha kushiriki ni Polisi, Mbuyuni, Nyuki, African Magic, stone town zote za Unguja pamoja na Tonado ya Kisiwani Pemba wakati kwa Tanzania JKT na timu ya Oilers ndizo zilizothibitisha mpaka sasa.


Na kwa upande wa Wanawake timu zilizothibitisha ni KVZ, African Magic, Mafunzo zote za Unguja ambapo kwa Pemba ipo Chake stars na kwa Tanzania Bara kuna JKT na oilers.
Kikosi cha African Magic
 

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE