LIGI KUU ZENJ BADO INAWAKA MOTO MKALI, KMKM HOI KWA MAOSTADHI WA CHUONI

Wachezaji wa KMKM

Ligi kuu soka ya Zanzibar kanda ya Unguja imeendelea tena leo kwa kupigwa michezo miwili tofauti ambapo saa 8:00 za mchana katika Uwanja wa Amaan  mabaharia wa KMKM wakakubali kuchapwa bao 1-0 dhidi ya Maostadhi wa Chuoni.

Mchezo mwengine umepigwa saa 10 za jioni kiwanjani hapo baada ya Mafunzo kuichapa Kijichi 2-0.

Lakini kwa upande wa kanda ya Pemba leo Chipukizi ilitoka na ushindi mabao 5-1 dhidi ya Aljazeera huku Shaba wakiichapa New Star bao 1-0.

Ligi kuu soka ya Zanzibar kanda ya Unguja itaendelea tena kesho kwa kupigwa michezo miwili katika Uwanja wa Amaan.

Saa 10:00 za jioni Mundu FC v/s Chwaka Stars, na saa 1:00 usiku ni zamu ya Polisi v/s Zimamoto.

Mzunguko wa 32 utamalizika Jumanne 25-04-17        Miembeni SC v/s Kilimani City FC      Amani saa 8:00 mchana, na saa 10:00 za jioni KVZ v/s Black Sailors na saa 1:00 Usiku Derby ya Jangombe kati ya Jang’ombe Boys FC v/s Taifa ya Jang’ombe.


Comments

Popular posts from this blog

HUYU NDIYE MCHEZAJI MWENYE REKODI YA KUFUNGA MAGOLI MENGI KWENYE MECHI YA TAIFA DHIDI YA BOYS