MAXMILIANA WA TAEKWON-DO AWAPA TANO WAANDISHI WA HABARI

Wachezaji wa mchezo wa Taekwon-do 
Kocha mkuu wa mchezo wa Taekwon-do Zanzibar Maxmiliana Kailangana ametoa shukrani zake za dhati kwa Waandishi wa Habari baada kuusambaza mchezo huo na kuanza kujulikanwa katika Visiwa vya Zanzibar.

Maxmiliana amesema kwasasa wana zaidi ya Wachezaji 15 wapya ambao wamevutiwa kujiunga na mchezo huo huku akisisitiza bila ya Vyombo vya Habari mchezo huo usengejulikanwa.

“Tunawashukuru Waandishi wa Habari wote ambao wamekuwa nasisi tangu tunaanzisha mchezo huo hapa Visiwani, maendeleo kwasasa ni mazuri kwani idadi ya wachezaji imezidi na sasa tumewapata zaidi ya wachezaji 15 wapya ambao wamevutiwa na mchezo huu”. Alisema Maxmiliana.

Taekwon-do ni mchezo mpya kwa Zanzibar ambapo asili yake ni nchini Korea kwa lugha nyepesi unaweza ukauwita sanaa ya mapambano ambapo wenzetu Tanzania bara mchezo huu si mgeni lakini katika Visiwa hivi ndo kwanza unaanza kuanzishwa na kusambazwa kwani wengi wanaufananisha na mchezo wa karati lakini ni tofauti kabisa licha ya kuwa mchezo huo pia wanatumia kupiga mateke na kurusha ngumi .

Mchezo huo unafundishwa katika ukumbi wa Judo Amani Mjini Zanzibar na Kocha Maxmiliana Kailangana ambae katokea Tanzania bara sasa yupo hapa Zanzibar kuusambaza mchezo huo kwa kila siku ya Jumatatu, Jumatano na Alhamis kuanzia saa 1:00 usiku hadi 3:00 usiku.


Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE