MFAUME APATA SHAVU KUCHEZESHA MECHI YA KIMATAIFA

Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF), limemteua Mfaume Ali Nassor wa Zanzibar kuwa mwamuzi wa kati katika mchezo wa Kimataifa wa kugombea CHAN utakaozikutanisha timu za taifa za Sudani ya Kusini dhidi ya Somalia utakaofanyika April 22, 2017 huko Djibouti na umelazimika kuchezwa huko kwa vile wenyeji Somalia nchini kwao bado hakujatulia.

Kwa mujibu wa taarifa ya CAF iliyofika Chama cha Soka Zanzibar (ZFA) mapema wiki hii, pia imewataja waamuzi wasaidizi ambao wanatoka Tanzania bara.

Waamuzi hao ambao ni washika vibendera ni Ferdinand Chacha, Frank Komba wakati mezani atakuwa Israel Nkongo huku Kamishna wa mchezo huo atatoka Kenya ambaye anaitwa Edil Likono.


Mfaume Ali Nassor ni miongoni mwa Waamuzi wenye Beji ya Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) kutoka Zanzibar.
Mfaume Ali Nassor 

Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE