MFUMO GANI WA KUPATIKANA TIMU 12 ZA MSIMU UJAO, MKUTANO MKUU WA ZFA UTAKAOFANYIKA JUMAMOSI PEMBA UTAJADILI



Mkutano Mkuu wa dharura wa ZFA TAIFA unatarajiwa kufanyika Siku ya Jumamosi ya April 22, 2017 katika Ukumbi wa Uwanja wa Gombani Kisiwani Pemba kuanzia saa 3:00 za asubuhi.

Katika Mkutano huo zitajadiliwa Ajenda 5 na mengineyo kati ya hizo ajenda ikiwemo kuhusu maboresho ya Katiba ya ZFA kuendana na matakwa ya Shirikisho la Soka Barani Afrika “CAF” ambapo hivi karibuni Zanzibar imekuwa mwanachama wa 55 wa Shirikisho hilo.

Mbali na ajenda hiyo, pia ajenda kubwa zaidi inayosubiriwa kwa hamu kubwa sana na wadau wa soka Zanzibar ni ajenda nambari 4 kuhusu mfumo gani utatumika kuzipata timu 12 ambazo zitashiriki ligi kuu soka ya Zanzibar kwa msimu ujao wa mwaka 2017 -2018 ambapo kwa msimu huu ligi hiyo ina jumla ya vilabu 36 kwa kanda zote za Unguja na Pemba, ambapo katika Ajenda hiyo Umoja wa vilabu watatoa pendekezo kuhusu upatikanaji wa timu 12 za premier.

Ajenda zitakazojadiliwa hizo:-
1.      Kupokea taarifa kuhusu uanachama kamili wa zfa kutoka CAF.
2.      Kupokea taarifa ya mjumbe wa kamati tendaji kutoka wilaya ya Kaskazini “A” na mjumbe kutoka wilaya ya Mjini.
3.      Kupokea taarifa ya uteuzi wa Mkurugenzi wa ufundi (Technical director).
4.      Kupokea pendekezo kutoka umoja wa vilabu kuhusu upatikanaji wa timu 12 za premier.
5.      Kuunda kamati ndogo ya watu wasiozidi 3 ambao wataifanyia marekebisho katiba ya zfa kwa ajili ya kwenda sambamba na matakwa ya fifa na caf kwa mujibu wa mazingira ya Zanzibar.
6.      mengineyo.

Wajumbe Kutoka Kisiwani Unguja wanatarajiwa kuondoka kesho kutwa Ijumaa kwa wale ambao watatumia njia ya Bahari na wale wajumbe wengine watakaotumia njia ya anga wataondoka siku hiyo hiyo ya Jumamosi asubuhi.


Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE