MIEMBENI CITY YAITAKA LIGI KUU KWA HAMU KUBWA

Timu ya Miembeni city imefanikiwa kupata alama tatu muhimu jioni ya leo baada ya kuifunga timu ya Sebleni United katika mchezo wa 4 bora ligi daraja la kwanza Taifa uliopigwa katika Uwanja wa Amaan.

Katika mchezo huo ambao ulikuwa na upinzani mkubwa mabao ya Miembeni City yamefungwa na Ahmed Keis dakika ya 79 na Issa Chitwanga dakika ya 84.

Mchezo mwengine umepigwa saa 1 za usiku katika uwanja huo wa Amaan ambapo timu ya Charawe ikafanikiwa kupata ushindi wa mabao 4-2.

Kwa matokeo hayo Miembeni City imezidi kujipa matumaini ya kupanda ligi kuu msimu ujao ambapo wakifanikiwa kupita hapo watakutana na timu nyengine ambazo zitabakia kwenye ligi kuu msimu huu pamoja na wao wanne wawili kutoka Pemba na wawili Unguja ili kupanga mfumo gani watumie kupatikana timu 12 za ligi kuu msimu ujao.

City mchezo wa awali waliichapa Charawe mabao 2-0 ambapo mpaka sasa wanaongoza wakiwa na alama 6 kwa michezo miwili huku Charawe ikishika nafasi ya pili kwa alama 3 na Ngome ikishika nafasi ya tatu pia ikiwa na alama 3 huku Sebleni United ikifuta matumaini ya kucheza ligi kuu msimu ujao kufuatia kufungwa michezo yote miwili ambapo wa awali ilichapwa 2-1 na Ngombe.

Michezo ya mwisho itapigwa Mei 9, 2017 ambapo saa 10:00 za jioni kumi watasukumana Sebleni United dhidi ya Charawe na saa 1:00 za usiku Miembeni City watamalizana na Ngome michezo yote itachezwa katika uwanja wa Amani mjini Unguja.


Wachezaji wa Miembeni City

Comments

Popular posts from this blog

HUYU NDIYE MCHEZAJI MWENYE REKODI YA KUFUNGA MAGOLI MENGI KWENYE MECHI YA TAIFA DHIDI YA BOYS