MIEMBENI WATIA AIBU LIGI KUU ZENJ, WAFIKA UWANJANI NA WACHEZAJI 9 TU

Timu ya Miembeni wazee wa kwala leo imeonesha kituko katika mchezo wa ligi kuu soka ya Zanzibar kanda ya Unguja baada ya kufika kiwanjani hapo wakiwa wachezaji 8 pekee.

Mchezo huo uliopigwa majira ya saa 8 za mchana katika uwanja wa Amaan ambapo Kwala walikuwa wanacheza na Mafunzo.

Mchezo umeanza huku Miembeni wakiwa pungufu (9) na baadae wakatimia 11, wakaenda mapumziko Mafunzo 3-0 Miembeni .

Waliporudi kipindi cha pili wakaingia 8 wakacheza mchezo huo mpaka dakika ya 54 Miembeni wakabakia wachezaji 6 uwanjani kufuatia wachezaji wake wengine wawili kushindwa kuendelea na mchezo, ndipo hapo Muamuzi Mfaume Ali Nassor kulazimika kuuvunja mchezo huo huku Mafunzo akiwa mbele kwa mabao 4-0.

Mchezo mwengine umepigwa saa 10 za jioni ambapo JKU akaifunga Mundu mabao 4-0.

Ligi hiyo itaendelea tena Jumanne.

J/nne 02/5 Chwaka vs Zimamoto saa 8:00 Amaan
J/nne 02/5 B/Sailors vs Kimbunga saa 10:00 Amaan
J/nne 02/5 Kilimani C vs J/Boys saa 1:00 usiku.

Jumatano 3/5 KMKM vs Malindi saa 8:00 Amaan.
Jumatano 3/5 Kipanga vs KVZ saa 10:00  Amaan.

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE