MKUTANO WA ZFA UMESHAANZA KUIBUA MAPYA
Viongozi wa wakuu wa ZFA wakiomba dua ya kuanza mkutano Mkuu |
Mkutano Mkuu wa dharura wa ZFA TAIFA unaendelea sasaivi hapa
Kisiwani Pemba katika Ukumbi wa Uwanja
wa Gombani tangu 3:00 za asubuhi.
Katika Mkutano huu zinajadiliwa Ajenda 5 na mengineyo kati ya
hizo ajenda ikiwemo kuhusu maboresho ya katiba ya ZFA kuendana na matakwa ya
Shirikisho la Soka Barani Afrika “CAF” ambapo hivi karibuni Zanzibar imekuwa
mwanachama wa 55 wa Shirikisho hilo.
Mbali na ajenda hiyo, pia ajenda kubwa zaidi inayosubiriwa
kwa hamu kubwa sana na wadau wa soka Zanzibar ni ajenda nambari 4 kuhusu mfumo
gani utatumika kuzipata timu 12 ambazo zitashiriki ligi kuu soka ya Zanzibar
kwa msimu ujao wa mwaka 2017 -2018 ambapo kwa msimu huu ligi hiyo ina jumla ya
vilabu 36 kwa kanda zote za Unguja na Pemba, ambapo katika Ajenda hiyo Umoja wa
vilabu watatoa pendekezo kuhusu upatikanaji wa timu 12 za premier.
Ajenda ambazo zinajadiliwa hizo:-
1. Kupokea taarifa
kuhusu uanachama kamili wa zfa kutoka CAF.
2. Kupokea taarifa
ya mjumbe wa kamati tendaji kutoka wilaya ya Kaskazini “A” na mjumbe kutoka
wilaya ya Mjini.
3. Kupokea taarifa
ya uteuzi wa Mkurugenzi wa ufundi (Technical director).
4. Kupokea
pendekezo kutoka umoja wa vilabu kuhusu upatikanaji wa timu 12 za premier.
5. Kuunda kamati
ndogo ya watu wasiozidi 3 ambao wataifanyia marekebisho katiba ya zfa kwa ajili
ya kwenda sambamba na matakwa ya fifa na caf kwa mujibu wa mazingira ya
Zanzibar.
6. mengineyo.
Katika mkutano huo kuna baadhi ya Wajumbe wanatarajiwa
kufukuzwa katika Chama hicho, zaidi endelea kufatilia Blog hii.
Wajumbe wa Mkutano Mkuu ZFA |
AsubscomWperfmu Jennifer Williams https://wakelet.com/wake/n1FL6t3pRB-6VXuzjrI6b
ReplyDeletelinkaeconsdis
eraqYfa_ga Megan Davis Avast Cleanup
ReplyDeleteWinRar
UltraISO
giosmaretun
graviqsper_wo Chris Kumar click
ReplyDeletenoifranutel