RAIS WA BOYS AVUNJA REKODI YAKE MWENYEWE, NA NDIE MCHEZAJI ALIYEMFUNGA MABAO MENGI KIPA SALULA WA TAIFA

Mshambuliaji hatari wa timu ya Soka ya Jang’ombe Boys Khamis Mussa (Rais) amevunja rekodi nyingine akiwa Boys katika Dabi ya Jang’ombe kati ya Jang’ombe Boys dhidi ya Taifa ya Jang’ombe.

Goli alilofunga jana katika dakika ya 86 dhidi ya Taifa ya Jang’ombe limemfanya kufikisha mabao matatu katika mchezo wa Dabi ya Jang’ombe kati ya Jang’ombe Boys dhidi ya Taifa ya Jang’ombe akicheza katika dimba Amaan, ambapo Boys kwa mara ya kwanza msimu huu wakiifunga Taifa baada ya kushinda 1-0.

Rais ameanza safari yake ya kufunga katika Dabi hiyo alipofunga mabao mawili kwenye mchezo wa mzunguko wa kwanza wa ligi kuu soka ya Zanzibar kanda ya Unguja ambapo timu hizo zilitoka sare ya kufungana mabao 2-2 mchezo uliopigwa katika Uwanja wa Amaan siku ya Jumamosi ya Disemba 10, 2016.

Rikodi nyengine aloiweka Rais jana amekuwa mchezaji wa kwanza kumfunga mabao mengi zaidi mlinda mlango hatari wa Taifa ya Jang’ombe Ahmed Ali “Salula” baada ya kumfunga mabao matatu kwenye msimu huu.

Baada ya kufunga bao hilo pekee jana Rais amefurahi sana huku akisema hafurahi kushinda yeye bao bali furaha yake kubwa ni kuwafunga Taifa ambao wamekuwa wanawapa tabu sana wakikutana nao.

“Leo (Jana) ni siku ya furaha sana kwangu, ninafuraha mpaka basi tena, sifurahi kushinda mimi bao, bali nafurahi kuwafunga Taifa, mana hao wanakuwa wanatupa tabu sana tukikutana nao, mechi hii inakuwa na upinzani mkubwa sana na mashabiki wanatoleana maneno mengi, sasa tumewaziba midomo, sisi ndio Boys, umoja wetu ndio siri ya mafanikio”. Alisema Rais.

Comments

Popular posts from this blog

HUYU NDIYE MCHEZAJI MWENYE REKODI YA KUFUNGA MAGOLI MENGI KWENYE MECHI YA TAIFA DHIDI YA BOYS