SQUASH KUMEKUCHA UCHAGUZI MEI





Chama cha Mpira wa Ukuta Zanzibar  “Zanzibar Squash Racket Association (ZSRA)”  kipo mbioni kufanya Uchaguzi wake ambao unatarajiwa kufanyika Mei 6, 2017 ambapo mpaka sasa haujajulikanwa utafanyika katika ukumbi gani.

Zoezi hilo litaanza harakati zake kuanzia April 17-19, 2017 ambapo fomu zitaanza kuchukuliwa kwenye Uwanja wa Squach uliopo Polisi Ziwani Mjini Unguja ambapo April 23, 2017 ndio mwisho wa kurejesha fomu wakati huo huo April 24 ni siku ya kutajwa majina ya Wagombea ambapo April 25 ni siku ya kupokea malalamiko na pingamizi ambapo April 26 ni siku ya kusikilizwa pingamizi, baada ya hapo April 27-28 watahojiwa wagombea na kamati hiyo na Mei 5, 2017 ni siku ya mwisho ya kupiga kampeni ambazo zitaanza tangu April 24.

Uchaguzi huo ambao utagombewa nafasi 6 zikiwemo Mwenyekiti, Makamo Mwenyekiti, Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu, Mshika Fedha na Mshika Fedha Msaidizi.

Kamati itakayosimamia Uchaguzi huo ina wajumbe 7 wakiongozwa na Mwenyekiti Abdallah Juma na Katibu Yussuf Mohd Ali “Kareka” huku wajumbe wakiwa Juma Mussa Rashid, Omar Makungu Omar, Mwanaidi Abdallah Makame, Zuhura Mohd Ali na Hadia Yahya Khamis.

Kamati hiyo imeweka hadharani sifa 6 za kuwa mgombea .
1.        Mgombea asipungue miaka 30.
2.        Mgombea awe amemaliza kidato kuanzia cha pili (Form II).
3.        Mgombea awe Mzanzibar.
4.        Mgombea awe hajawahi kufungwa.
5.        Mgombea awe ni mpenzi wa mchezo wa Squach.
6.        Mgombea awe na akili timamu.


Kwa mujibu wa katiba ya Chama hicho kila baada ya miaka 4 hufanyika Uchaguzi wa kuchagua viongozi wapya ambapo Uchaguzi uliopita ulifanyika mwaka 2012.

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE