TIMU 12 ZA LIGI KUU MSIMU UJAO KUPATIKANA BAADA YA KUMALIZIKA 8 BORA NDIPO VILABU 28 KUPANGA KWA PAMOJA

Viongozi wakuu wa ZFA


Wadau wengi wa soka Visiwani Zanzibar wanahamu sana kujua mfumo gani utatumika kwaajili ya kupatikana timu 12 za ligi kuu soka ya Zanzibar kwa msimu ujao wa mwaka 2017-2018.

Mkutano Mkuu wa dharura wa ZFA uliokaa asubuhi ya leo kwenye Ukumbi wa Uwanja wa Gombani Kisiwani Pemba umependekeza vilabu 28 vya ligi kuu ya Zanzibar msimu huu wakutane kwa pamoja baada ya kumalizika 8 bora na kupanga ni mfumo gani utumike ili zipatikane timu 12 za msimu ujao.

Timu hizo 28 ni zile ambazo zitanusurika kushuka daraja katika mkumbo wa awali ambapo hushuka timu 12 kwa kila kanda hushuka 6, yani Unguja 6 na Pemba.

Viongozi wa timu hizo 28 za Unguja na Pemba watakutana kwa pamoja baada ya kumalizika hatua ya 8 bora ambapo hapo ndipo patakapojulikanwa timu zipi zitacheza ligi kuu msimu ujao.

Hivyo pengine huwenda timu ikafanikiwa kuwa bingwa au Mshindi wa Pili wa Zanzibar (Wawakilishi wa Klabu Bingwa na Kombe la Shirikisho) lakini akashindwa kucheza ligi kuu ya Zanzibar kwa msimu ujao endapo akishindwa kuvuka katika  mfumo huo ambao utakaotumika.

Msimu huu wa mwaka 2016-2017 ligi kuu soka ya Zanzibar ina jumla ya timu 36 zikijumuisha 18 za Unguja na 18 za Pemba lakini ZFA baada ya kuwa mwanachama wa 55 wa Shirikisho la Soka Afrika “CAF”, Shirikisho hilo limekitaka chama hicho kuwa na vilabu 12 kwa msimu ujao wa mwaka 2017-2018.

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE