WAUZAJI KARAFUU ZSTC WAWATIA ADABU WAZIMA UMEME ZECO MASHINDANO YA MEI MOSI


TIMU YA SHIRIKA la Biashara la Taifa Zanzibar (ZSTC) imefanikiwa kutwaa ubingwa wa mwaka huu 2017 wa Mashindano ya Mei Mosi baada ya kuwafunga mabingwa Watetezi timu ya Shirika la umeme Zanzibar (ZECO) mabao 2-0 fainali ambayo imepigwa jioni ya leo katika Uwanja wa Amaan.

Mabao yote ya ZSTC yamefungwa na Majid Omar Majid ambae alionesha makali yake katika mchezo huo ambao ulitawaliwa na mvua kiwanjani hapo.

Katika Mashindano ya mwaka huu 2017 Mfungaji bora Bora amefanikiwa kuwa Habibu Juma Ali aliyefunga mabao 5 katika Mashindano hayo,  huku kipa bora akiwa Mbarouk Juma Ali wa Shirika la Bandari na Muamuzi bora ni Juma Makame.


Mashindano hufanyika kila mwaka na kuwapa fursa wafanyakazi wa Mashirika mbali mbali kuonesha viwango vyao.
Mh Ayoub Mohammed Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi akimkabidhi zawadi Juma Makame Muamuzi Bora

Comments

Popular posts from this blog

HUYU NDIYE MCHEZAJI MWENYE REKODI YA KUFUNGA MAGOLI MENGI KWENYE MECHI YA TAIFA DHIDI YA BOYS