COCA-COLA YAZIPIGA JEKI SHULE ZA SEKONDARI ZANZIBAR KWA KUWAPATIA JEZI NA MIPIRA


Kampuni ya vinyaji baridi ya Cocacola imetoa Vifaa vya Michezo vikiwemo jezi na mipira kwa ajili ya Skuli za Sekondari 251 za Unguja na Pemba kwa ajili ya michezo ya soka na mpira wa kikapu, pamoja na mashindano ya UMISSETA ambayo yatakayofanyika kuanzia June 6, 2017 huko Butimba Mkoani Mwanza ambapo Zanzibar mwaka  huu zitatoa kanda mbili tofauti, Kanda ya Unguja na Kanda ya Pemba.



Vifaa hivyo vimekabidhiwa na Waziri wa Habari, Utalii, Utamduni na Michezo Rashid Ali Juma ambae ndie aliyekuwa mgeni rasmi na ameipongeza kampuni hiyo kwa kuthamini Michezo huku akisisitiza kuvithamini na kuvitunza vifaa hivyo.

Mbali ya Vifaa hivyo pia Kampuni hiyo imetoa Vinywaji vya Coca cola kwa Wanafunzi na Wananchi wote waliyofika Uwanjani hapo Amaan kwenye hafla hiyo.
Afisa masoko msaidizi wa kampuni ya Cocacola Pamela Lugenge

Comments

Popular posts from this blog

HUYU NDIYE MCHEZAJI MWENYE REKODI YA KUFUNGA MAGOLI MENGI KWENYE MECHI YA TAIFA DHIDI YA BOYS