HATMA YA MALINDI, KIPANGA NA KILIMANI CITY NANI ATAUNGANA NA TIMU 5 KUSHUKA DARAJA LEO HUWENDA TUKAPATA KUJUA

Kikosi cha Kilimani City
Ligi kuu soka ya Zanzibar Kanda ya Unguja leo itaendelea tena kwa kupigwa michezo 3 katika viwanja viwili tofauti ambapo michezo hiyo inahusisha timu zote ambazo zipo hati hati kuungana na timu 5 kushuka daraja.

Timu 5 ambazo tayari zishajihakikishia kushuka daraja ni Kimbunga, Chaka Stars, Miembeni, Kijichi na Mundu ambapo wanaisubiri timu moja ili ziwe 6 kuungana kushuka daraja na homa kubwa ipo kwa vilabu vitatu ambavyo ni Malindi, Kipanga na Kilimani City na mmoja kati ya hao wataungana na vilabu vyengine vitano ambavyo tayari vishajihakikishia kushuka daraja.
Saleh Machupa kocha wa Malindi
MALINDI
Malindi imebakisha michezo 2 baada ya kucheza michezo 32 hadi sasa na kati ya michezo iliyosalia upande wao watacheza leo Jumatano 3/5 dhidi ya KMKM  saa 8:00 Amaan na mwengine watamalizana na Taifa ya Jang’ombe ambao watacheza Jumamosi 06-05-2017 saa10:00 Amaan.

Malindi ipo nafasi ya 13 wana alama 39 katika michezo 32 waliyocheza wameshinda 11 sare 6 na kupoteza 15.


Kikosi cha Kipanga

KIPANGA
Timu hii inamilikiwa na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) ambapo wamebakiwa na michezo miwili kati yao na KVZ utakaochezwa  leo Jumatano 3/5/2017 saa 10:00  Amaan, na mchezo wao wa mwisho watamalizana na KMKM Jumapili ya 07-05-2017 saa 1:00 USIKU Aman.

Katika Msimamo wapo nafasi ya 12 wakiwa na alama 41 kati ya michezo 32 waliyocheza wameshinda 12, sare 5 na wamefungwa 15.

KILIMANI CITY
Kilimani City wenyewe wanajita watoto wa Mjini wamebakiwa na michezo 2 , mmoja watacheza leo Jumatano 03/5/2017 dhidi ya Jang’ombe Boys saa 10:00 jioni katika uwanja wa Fuoni, na wa mwisho watamalizana na Chuoni Tarehe 05-05-2017 saa 1:00 za usiku Amaan.

Katika msimamo wapo nafasi ya 11 katika michezo 32 waliyocheza wameshinda 13, sare 4 na kupoteza 15.

Kati ya Malindi, Kipanga na Kilimani City nani ataungana na Kimbunga, Chaka Stars, Miembeni, Kijichi na Mundu kushuka Daraja?, jawabu lake huenda tukaanza kulipata jioni ya leo baada ya kumalizika kwa michezo yote hiyo mitatu.

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE