HIYO NDO NEMBO MPYA YA ZFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF


Chama cha soka Visiwani Zanzibar kimefanya marekebisho ya nembo yao na sasa watatumia nembo hiyo (Pichani) katika shughuli zao zote za Chama hicho.

Siku ya Alhamis Machi 16, 2017 itaendelea  kukumbukwa na Wazanzibar baada ya ZFA kuingizwa rasmi kuwa Mwanachama wa 55 wa Shirikisho la Soka Barani Afrika “CAF” kufuatia Kikao cha 39 cha Mkutano Mkuu wa Shirikisho hilo kilichofanyika Addis Ababa nchini Ethiopia.

Katika kura 54 za CAF, kura 51 zimekubali Zanzibar ipatiwe uanachama wa kudumu wa Shirikisho hilo na nchi 3 zilikataa Zanzibar isipatiwe ambazo ni Madagascar, Benin na Seychelles.


Tangu viongozi wa ZFA pamoja na Waziri wa Habari Utalii Utamaduni na Michezo Zanzibar Rashid Ali Juma warejee Visiwani Zanzibar wakitokea huko Addis Ababa katika mkutano huo, ZFA wakaanza kazi ya kuirekebisha nembo yao.
Nembo ya ZFA ya Zamani

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE