JE UNAJUA KUWA TIMU 12 ZILIZOSHUKA LIGI KUU YA ZENJ ZOTE ZA URAIANI?

Kikosi cha Miembeni
Ikiwa ligi kuu soka Zanzibar imemaliza hatua ya awali na ikisubiri kuanza 8 bora Jumamosi hii huku timu 12 za uraini zashuka daraja.

Ligi kuu soka ya Zanzibar msimu huu wa mwaka 2016-2017 ulikuwa una jumla ya timu 36 kwa kila kanda timu 18, yani kanda ya Unguja 18 na Pemba 18.

Katika vilabu hivyo 36, klabu za Uraiani vilikuwa 28 huku timu za Vikosi zilikuwa 8.

Timu hizo 8 za Vikosi ni JKU, Zimamoto, KMKM, Mafunzo, KVZ ambavyo ni Vikosi vya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) , vyengine ni Polisi, Kipanga na Hardrock (JWTZ) vyote vikitoka Serikali ya Jamhuri ya Muungano Tanzania.

Timu 12 zilizoshuka daraja kutoka ligi kuu hadi Daraja la Kwanza Taifa kutoka Unguja ni Malindi, Kijichi, Mundu, Miembeni, Chwaka stars na Kimbunga wakati zile za Pemba ni Maji maji, Sharp Victor, Aljazira, Danger Boys, African Kivumbi, na Madungu.

Uwepo wa Vilabu vingi vya Mitaani hasa vinavyotoka kwenye mitaa husika kama vile Chwaka, Miembeni,  Malindi,  Madungu na Kijichi vilitegemewa vitafanya vizuri katika ligi hiyo kwa vile vimebeba jina la mtaa husika lakini mwisho wa ligi vimeteremka daraja.

Na: Mossi Abdallah, Zanzibar.
Kikosi cha Chwaka Stars

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE