JIMBO LA KIKWAJUNI LAUNGANA NA MALINDI NA KWAHANI NUSU FAINALI

Ligi ya Majimbo imeendelea tena jioni ya leo Jumamosi katika uwanja wa Polisi Ziwani huku tukishuhudia Jimbo la Kikwajuni kutinga hatua ya nusu baada ya kulitoa jimbo la Mfenesini kwa penalti 5-4 kufuatia dakika 90 kumalizika kwa sare ya 0-0.


Kikwajuni wataungana nusu fainali na Jimbo la Malindi na Kwahani wakimsubiri mshindi wa robo fainali ya mwisho itakayopigwa kesho saa 10 katika Uwanja wa Polisi Ziwani kati ya Timu ya Afisi kuu ya CCM dhidi ya timu ya Kaskazini.

Bingwa wa Mashindano hayo ya Majimbo atazawadiwa Gari aina ya Carry.

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE