KAMPUNI YA SANSI YAIPIGA TAFU TIMU YA GULIONI KWA KUIDHAMINI ASILIMIA 60

Suhail Suleiman Mkurugenzi wa Kampuni ya SANSI


 Kampuni ya SANSI inayomiliki Viwanda na Ukodishaji wa Nyumba hapa Zanzibar imeidhamini kwa asilimia 60 klabu ya Gulioni FC inayoshiriki ligi daraja la Pili Wilaya ya Mjini Unguja.


Akizungumzia lengo la kuidhamini timu hiyo Suhail Ibrahim ambae ni Mkurugenzi wa Kampuni hiyo amesema kikubwa kilichomvutia mpaka kampuni yake ikaidhamini Gulioni kwakuwa timu hiyo inamvuto mkubwa sana na hamasa ya Mashabiki wake.

“Kampuni yangu imevutiwa na hamasa ya Mashabiki wa Gulioni, ndio maana nikaamua kuidhamini timu hii, udhamini wetu ni kwa asilimia 60 timu itaidhamini na huko mbele ikiwa mambo yatakwenda vizuri tutazidi kuidhamini kwa asilimia kubwa zaidi”. Alisema Suhail.


Wachezaji wa Gulioni FC
Nae Ahmed Khamis ambae ni Rais wa Gulioni FC ameishukuru sana Kampuni hiyo kwa udhamini wao huku akiwaahidi Mashabiki wa Gulioni watazidi kufanya vizuri katika hatua ya 4 bora baada ya udhamini huo.

“Tunaishukuru Kampuni ya SANSI kwa udhamini wao, kwani kuna vilabu vingi kaviacha kaja kwetu Gulioni, tunawashukuru sana na pia tunawakaribisha na tutafanya kazi vizuri ili lengo letu litimie, naamini katika hatua ya 4 bora inayoendelea tutazidi kuwa bora baada ya udhamini huu”. Alisema Ahmed.
Rais wa Gulioni Ahmed Khamis akikabidhiwa Jezi na mdhamini wao

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE