KIKOSI KIPYA CHA KOMBAIN YA MJINI ROLLING STONE CHAKUTANA LEO


Kikosi  cha wachezaji 37 cha Kombain Wilaya ya Mjini ambacho kinatarajiwa kwenda Arusha katika Mashindano ya Vijana ya Afrika Mashariki ya Rolling Stone kimekutana asubuhi ya leo na viongozi wa timu yao inayoongozwa na Kocha Mkuu Mohammed Seif “King” .

Wachezaji hao wamekutana katika Ukumbi wa Uwanja wa Amaan ambapo wameenda kujuana na kisha kupanga mikakati yao ya kuanza mazoezi ambapo wakitarajiwa kufanya mazoezi kila siku ya Jumamosi na Jumapili asubuhi katika Uwanja wa Amaan.

Benchi la Ufundi la timu hiyo linaongozwa na Kocha Mkuu Mohammed Seif “King”, Kocha Msaidizi Ramadhan Abdul rahman “Madundo”, Meneja wa Timu Ali Othman “Kibichwa”, Kocha wa Makipa Salum Ali “Chulas” na Mtunza vifaa Nassir Kheir.

Wachezaji 37 wa awali waliotangazwa wiki iliyopita ni:-

Walinda Mlango ni Rajab Farouk Festo (Real Kids), Peter Dotto Mashauri (Schalke 04) na Makame Mkadar Koyo (Huru).

Wachezaji wa ndani ni Hassan Chalii (Kipanga), Abdul-halim Ameir (King Boys), Mahad Hassan Bai (Kijangwani), Yahya Silver (Muembe ladu), Shaaban Pandu (Villa United), Saleh Khatib (Kijangwani), Idrissa Makame (Villa FC), Ramadhan Simba (Calypso), Khatib Kombo (Schalke 04), Othman Jumbe (Black Sailors), Ali Hassan (Uhamiaji), Fahmi Salum (Mlandege), Salum Omar (Villa United), Yakoub Omar (Jang’ombe Boys), Nassir Ramadhan (Muembe Makumbi) na Mohd Ridhaa (Villa United).

Wengine ni Mussa Shaaban (Zimamoto), Ismail Kassim (Huru), Seif Said (KVZ), Abdillah Suleiman (King Boys), Haji Suleiman (JKU), Mohd Jailan (Chrisc), Makame Maoud (Schalke 04), Fahad Mussa (Mapembeani), Mohd Mussa (Mapembeani), Abrahman Juma (KMKM), Suleiman Dorado (Uhamiaji), Said Salum (Real Kids), Mohd Haji (Jang’ombe Boys), Abrahman Juma (ZAFSA), Abdul-hamid Juma (ZAFSA), Khatib Ameir (Real Kids), Yussuf Mohd (Muembe Beni) na Ibrahim Chafu (Villa FC).


Mashindano ya Rolling Stone yatafanyika Jijini Arusha mwezi July, 2017 ambapo awali yalikuwa yafanyike Nairobi nchini Kenya lakini kutokana na Uchaguzi wa nchi uliopo huko umelazimika kuyarejesha tena Arusha yalipofanyika mwaka jana.
Wachezaji wa Wilaya ya Mjini

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE