KILIMANI CITY YAPANIA KUMLETA KOCHA KUTOKA MISRI, MAZUNGUMZO YAO YAMEFIKIA PAZURI

Mohammed Mbaraka "Mebo" 

Baada ya kunusurika kushuka daraja kwenye mkumbo wa awali ligi kuu soka ya Zanzibar, klabu ya Kilimani city imepania kumleta kocha kutoka nchini Misri ambae ni Mohammed Mbaraka “Mebo”na mazungumzo yamefikia patamu kati yao.

Akizungumza na kisanduzenj.blogspot.com Rais wa Kilimani City Khamis Shaali amesema wameshaanza mazungumzo na kocha huyo na tayari wasifu wake ameshawatumia (CV) na uongozi wao City wameridhika na sifa za mwalimu huyo.

Amesema wanatarajia kumleta kocha Mebo ambae ana leseni B ya Shirikisho la Soka Afrika na msimu mpya ukianza kocha huyo ataonekana katika soka la Zanzibar akiwa na klabu ya Kilimani city.

“Mipango yetu na kocha Mohammed Mubarak yanakwenda vizuri na msimu ujao tutakuwa nae ligi ikianza kocha huyu ni kutoka Misri, na tayari kashatuma CV zake kama unavyoziona hapa, anasifa nyingi sana nzuri na tumeipenda CV yake”, Alisema Shaali.

Katika ligi kuu soka ya Zanzibar kanda ya Unguja Kilimani City imenusurika kushuka daraja katika mkumbo wa awali baada ya kumaliza ikiwa nafasi ya 11 wakiwa na alama 47 kwa michezo 34 ya ligi hiyo.


City ni miongoni mwa timu 28 za Unguja na Pemba ambazo zitapigania katika kinyanganyiro cha kutafuta timu 12 ambazo zitacheza ligi kuu msimu ujao, msimu ambao zinatakiwa timu 12 tu pekee, baada ya kumalizika hatua ya 8 bora, hapo ndipo patakapojulikanwa timu zipi zitacheza ligi kuu msimu huo na mfumo gani utumike kupatikana kwa timu hizo 12 baada ya kukaa kwa pamoja viongozi wa timu hizo 28 na kupanga mfumo gani watumie ili wazipate timu hizo 12.

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE