KIPANGA YAISHUSHA DARAJA MALINDI

Leo rasmi timu ya Malindi imeungana na Kimbunga, Chwaka Stars, Miembeni, Kijichi na Mundu kushuka daraja kutoka ligi kuu hadi ligi daraja la Kwanza baada ya jioni ya leo Kipanga kutoka sare ya 2-2 dhidi ya KMKM katika mchezo wa mwisho wa ligi kuu soka ya Zanzibar kanda ya Unguja uliopigwa katika uwanja wa Amaan.

Kwa matokeo hayo Kipanga imemaliza ligi hiyo salama ikiwa na alama sawa na timu ya Malindi iliyoshuka daraja wote wana point 42 lakini Kipanga ana faida ya mabao baada ya kuwa na akiba ya mabao 4 huku wenzao Malindi wana deni la mabao 7 na kusababisha kushuka daraja.

Mchezo mwengine leo KVZ wakaitandika Kimbunga mabao 6-1 uliosukumwa saa 8 za mchana katika Uwanja wa Amaan huku Kijichi wakaichapa Chwaka Stars 1-0 mchezo uliopigwa majira ya saa 10 za jioni Fuoni .

Sasa ligi hiyo leo imemaliza rasmi na inatarajiwa Jumamosi ijayo kuanza hatua ya 8 bora ambapo timu 4 za Unguja zilizotinga hatua hiyo ni JKU, Jang’ombe Boys, Zimamoto na Taifa ya Jang’ombe huku za Pemba ni Jamhuri, Mwenge, Kizimbani na Okapi zote kutoka mkoa wa kaskazini Pemba.
Kikosi cha Kipanga

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE