KOCHA WA ZANZIBAR HEROES AREJEA ZENJ AKITOKA CAMEROON KWENYE KOZI YA CAF YA MAGOLIKIPA


Kocha wa Makipa wa timu ya Taifa ya Zanzibar (Zanzibar Heroes) ambae pia ni kocha Mkuu wa timu ya Malindi Saleh Ahmed Seif “Machupa” amerejea Visiwani Zanzibar akitokea Cameroon kwenye Kozi ya CAF ya Wakufunzi wa Makocha wa Magolikipa iliomaliza mwishoni mwa wiki iliyopita.

Katika kozi hiyo ya Wakufunzi wa Makocha wa Magolikipa iliyofanyika wiki moja huko Cameroon Machupa amefanikiwa kuhitimu vyema na sasa atakuwa Mkufunzi rasmi wa Makocha wa Magolikipa Zanzibar.


Mara baada ya kuwasili tu visiwani Zanzibar Blog ya kisanduzenj.blogspot.com imefanikiwa kumnasa kocha huyo na akielezea kozi hiyo ilivyokuwa.

“Kozi ilikuwa si nyepese lakini nashkuru kumaliza salama na kufanikiwa, hivyo sasa nimefanikiwa kuwa Mkufunzi rasmi wa Makocha wa Magolikipa ndani ya nchi yangu, Wakufunzi wengine wanasomesha nchi yoyote Afrika lakini mimi kiwango changu cha awali natakiwa kusomesha Zanzibar, hivyo kwa msimu ujao makocha wa Magolikipa wanatakiwa wawe na japo kozi ya Msingi wakikaa kwenye benchi ndani ya ligi kuu, hivyo nawaomba makocha wenzangu tujiendeleze kusoma pindi tunaposikia nafasi zimetoka kwani huko mbele tunapokwenda ni kugumu mno, na mimi natarajia kuendesha hiyo kozi”. Alisema Machupa.


Mbali ya kuhitimu kuwa Mkufunzi wa ndani, Machupa pia ameshahitimu kozi ya FIFA ya Ukocha wa Magolikipa ya hatua ya juu (Advanced Level) ambayo aliipata kwenye kozi iliyofayika tarehe 01 Agost, 2016 na kumalizika tarehe 05 Agost 2016, na pia Machupa ana Leseni “B” ya Ukocha inayotambuliwa na CAF.

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE