MADUNDO ATANGAZA KIKOSI KIPYA CHA WILAYA YA MJINI, WALOCHUKUA UBINGWA WOTE WAPIGWA CHINI KASORO MMOJA TU

Ramadhan Abdurahman "Madundo"
Kocha msaidizi wa Kombain ya Vijana Wilaya ya Mjini Ramadhan Abdurahman “Madundo” leo ametangaza kikosi kipya cha timu hiyo ambacho kinatarajiwa kwenda Arusha katika Mashindano ya Vijana ya Afrika Mashariki ya Rolling Stone yanayotarajiwa kufanyika July, 2017.

Mbali na kutangaza kikosi cha wachezaji 37, Madundo ametaja vipaombele vyake kwenye timu hiyo ambavyo amezingatia katika kuteua majina hayo.

Amesema kitu pekee ambacho wameangalia ni uwezo wa mchezaji na nidhamu ndani na nje ya uwanja ili kuweza kujenga timu imara ambayo itakuwa na uwezo wa kupambana kwa kuwawakilisha Zanzibar katika Mashindano hayo.


Aidha Madundo amesema katika Kikosi hicho wameamua kuwaacha wachezaji wote waliotwaa Ubingwa msimu ulopita Jijini Arusha na kuwemo mmoja tu ambae ni Abdurahman Juma “Baby” wa KMKM huku sababu kuu akisema kuwa umri wao umekuwa mkubwa ndio mana wamelazimika kutowajumuisha.

Kikosi kipya cha Kombain ya Mjini ni:-

Walinda Mlango ni Rajab Farouk Festo (Real Kids), Peter Dotto Mashauri (Schalke 04) na Makame Mkadar Koyo (Huru).

Wachezaji wa ndani ni Hassan Chalii (Kipanga), Abdul-halim Ameir (King Boys), Mahad Hassan Bai (Kijangwani), Yahya Silver (Muembe ladu), Shaaban Pandu (Villa United), Saleh Khatib (Kijangwani), Idrissa Makame (Villa FC), Ramadhan Simba (Calypso), Khatib Kombo (Schalke 04), Othman Jumbe (Black Sailors), Ali Hassan (Uhamiaji), Fahmi Salum (Mlandege), Salum Omar (Villa United), Yakoub Omar (Jang’ombe Boys), Nassir Ramadhan (Muembe Makumbi) na Mohd Ridhaa (Villa United).

Wengine ni Mussa Shaaban (Zimamoto), Ismail Kassim (Huru), Seif Said (KVZ), Abdillah Suleiman (King Boys), Haji Suleiman (JKU), Mohd Jailan (Chrisc), Makame Maoud (Schalke 04), Fahad Mussa (Mapembeani), Mohd Mussa (Mapembeani), Abrahman Juma (KMKM), Suleiman Dorado (Uhamiaji), Said Salum (Real Kids), Mohd Haji (Jang’ombe Boys), Abrahman Juma (ZAFSA), Abdul-hamid Juma (ZAFSA), Khatib Ameir (Real Kids), Yussuf Mohd (Muembe Beni) na Ibrahim Chafu (Villa FC).

Jumapili ya Mei 7, 2017 benchi la Ufundi la timu hiyo linaloongozwa na Kocha Mohammed Seif “King”  litakutana na wachezaji wote walioteuliwa kuanzia saa 4:00 za asubuhi kwenye Afisi ya ZFA Wilaya ya Mjini, Aman ili kuzungumza nao na kupanga utaratibu wa kuanza mazoezi.

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE