MALINDI, KIPANGA NA KILIMANI CITY NANI ATAUNGANA NA TIMU 5 KUSHUKA DARAJA


Zikiwa zimesalia mechi 2 kwa kila timu kati ya timu tatu zilizo katika vita ya kuepuka kushuka daraja ni wazi Ligi Kuu ya Zanzibar kanda ya Unguja msimu huu ina ushindani mwingine mkubwa chini ya msimamo kuliko katika mbio za kutinga 8 bora,  JKU, Jang’ombe Boys na Taifa ya Jang’ombe wameshajihakikishia kutinga hatua hiyo huku ikisubiriwa Zimamoto au Polisi ambapo Zimamoto inapewa nafasi kubwa kufuzu 8 bora.

Homa kubwa ipo kwa vilabu vitatu ambavyo ni Malindi, Kipanga na Kilimani City na mmoja kati ya hao wataungana na vilabu vyengine vitano ambavyo tayari vishajihakikishia kushuka daraja.

Timu 5 ambazo tayari zishajihakikishia kushuka daraja ni Kimbunga, Chaka Stars, Miembeni, Kijichi na Mundu ambapo wanaisubiri timu moja ili ziwe 6 kuungana kushuka daraja.

MALINDI
Malindi imebakisha michezo 2 baada ya kucheza michezo 32 hadi sasa na kati ya michezo iliyosalia upande wao watacheza kesho kutwa Jumatano 3/5 dhidi ya KMKM  saa 8:00 Amaan na mwengine watamalizana na Taifa ya Jang’ombe ambao watacheza Jumamosi 06-05-2017 saa10:00 Amaan. 

Malindi ipo nafasi ya 13 wana alama 39 katika michezo 32 waliyocheza wameshinda 11 sare 6 na kupoteza 15.
KIPANGA
Timu hii inamilikiwa na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) ambapo wamebakiwa na michezo miwili kati yao n KVZ utakaochezwa  kesho kutwa Jumatano 3/5/2017 saa 10:00  Amaan, na mchezo wao wa mwisho watamalizana na KMKM Jumapili ya 07-05-2017 saa 1:00 USIKU Aman.

Katika Msimamo wapo nafasi ya 12 wakiwa na alama 41 kati ya michezo 32 waliyocheza wameshinda 12, sare 5 na wamefungwa 15.

KILIMANI CITY
Kilimani City wenyewe wanajita watoto wa Mjini wamebakiwa na michezo 2 , mmoja watacheza kesho Jumanne 02/5/2017 dhidi ya Jang’ombe Boys saa 1:00 usiku Amaan, na wa mwisho watamalizana na Chuoni Tarehe 05-05-2017 saa 1:00 za usiku Amaan.

Katika msimamo wapo nafasi ya 11 katika michezo 32 waliyocheza wameshinda 13, sare 4 na kupoteza 15.
Kikosi cha Kipanga

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE