MASHINDANO YA RIADHA YA AFRIKA MASHARIKI NA KATI YASUKUMWA MBELE, ZANZIBAR WASEMA WATAZIDI KUJIPANGA UPYA

Chama cha Riadha Zanzibar kimepokea barua ya kutoka Shirikisho la Riadha Tanzania (RT) kwa kupelekwa mbele Mashindano ya Riadha kwa Vijana U-17 ya Afrika Mashariki na Kati ambayo yalikuwa yafanyike kesho na kesho kutwa Jijini Dar es salam.

Katibu wa Riadha Zanzibar Suleiman Ame amethibitisha kupokea taarifa hiyo kutoka kwa RT ambapo amesema Mashindano hayo yamesogezwa mbele mpaka Mei 13-14, 2017 jijini Dar es salam.

“Tumepokea Barua kutoka kwa RT kuwa mashindano yamesogezwa mbele, lakini sisi tutazidi kujipanga mana mazoezi tunaendelea kufanya asubuhi na jioni katika uwanja wa Amaan, sasa kusogezwa mbele inaweza kutusaidia zaidi kufanya vizuri sisi kama Zanzibar”. Alisema Ame.

Mpaka sasa nchi tano tu zimeshathibitisha kushiriki Mashindano hayo katika nchi 11 wanachama wakiwemo wenyeji Tanzania Bara, Zanzibar, Kenya, Uganda na Sudani ya Kusini.




Wachezaji wa Riadha Zanzibar mwaka jana waliporejea nyumbani katika Mashindano ya Vijana

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE