MIEMBENI CITY MABINGWA DARAJA LA KWANZA, WAICHUNGULIA LIGI KUU WAO NA CHARAWE
![]() |
Wachezaji wa Miembeni City wakiongozwa na Captain wao Habibu Ali (Wa pili Kulia) |
Mabao ya City yamefungwa na Yahya Karoa na Haruna Abdallah “Boban”
ambayo yamepeleka furaha klabuni kwao.
Kwa matokeo hayo City imefanikiwa kuongoza 4 bora na kutwaa
kombe la daraja la kwanza Taifa Unguja baada ya kufikisha alama 9 kwa michezo
mitatu kufuatia mchezo wa awali kuichapa Charawe 2-0, wakaipiga Sebleni United
2-0, na kuwamaliza Ngome 2-0, hivyo City wataungana na Charawe kuinusa ligi kuu
msimu ujao.
Mapema Charawe imefanikiwa kuondoka kwenye daraja la kwanza
Taifa na kusubiri mfumo gani utumike ili zipatikane timu 12 za msimu ujao wa
mwaka 2017-2018, baada ya kupata ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Sebleni United
kwenye hatua ya 4 ligi daraja la kwanza Taifa mchezo uliopigwa katika uwanja wa
Amaan.
Mabao ya Charawe yamefungwa na Is haka Mzee dakika ya 55,
Jumanne Abdallah dakika ya 60 na 71.
Timu 2 za juu kwa daraja la kwanza Taifa kwa kila Kanda
(Unguja na Pemba) yani Miembeni City na Charawe kwa Unguja, na zile mbili za
Pemba zitaungana na timu 24 zilizobakia kwenye ligi kuu na zitakuwa jumla ya
timu 28 kwa Zanzibar nzima, ndipo hapo kwa pamoja watapanga ni mfumo gani
utumike ili zipatikane timu 12 za msimu ujao ambapo inasubiriwa imalizike 8
bora ndipo mchakato huo uanze.
Wachezaji wa Charawe wakisalimiwa na Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Mh Ayoub Mohammed |
Comments
Post a Comment