MLANDEGE NA GULIONI HAPATOSHI KESHO

Kesho kutakuwa na Dabi kati ya Gulioni dhidi ya Mlandege kwenye mchezo wa ligi daraja la pili Wilaya ya Mjini hatua ya 4 bora mzunguko wa pili mchezo utakaochezwa saa 1:00 za usiku katika uwanja wa Amaan.

Mlandege walifungwa 1-0 na Gulioni walipokutana katika hatua ya 8 bora ambapo bao pekee la Gulioni lilifungwa na Mussa Haji Mussa,  hivyo mchezo wa kesho utakuwa na upinzani mkubwa kutokana na Mlandege kutaka kulipa kisasi na Gulioni kutaka kuendelea kutunza heshima.

Katika ligi hiyo timu zote 4 Kwerekwe City,  Amani Fresh,  Mlandege na Gulioni zina alama 1 kufuatia mchezo wa awali City kwenda sare ya 1-1 na Gulioni, Mlandege nae akatoka sare ya 1-1 na Amani Fresh.

Mchezo mwengine utapigwa Jumatano ya Mei 10, 2017 kati ya Kwerekwe City dhidi ya Amaan Fresh.

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE