MLANDEGE YAFUFUA MATUMAINI YA KWENDA MABINGWA WILAYA

Timu ya Mlandege jana usiku imefanikiwa kuongoza katika hatua ya 4 bora ligi daraja la Pili Wilaya Mjini baada ya kushinda mabao 3-1 dhidi ya Gulioni mchezo uliopigwa katika Uwanja wa Amaan.

Mabao ya Mlandege yamefungwa na Mohd Abdallah "Edo" dakika ya 47 na 66 na jengine likimalizwa na Hassan Ramadhan dakika ya 68.

Bao pekee la Gulioni limefungwa na Shaabani Hassan dakika ya 28.

Kwa matokeo hayo Mlandege anaongoza akiwa  na alama 4 kwa michezo miwili huku Amani Fresh na Kwerekwe City wakiwa na alama 1 kwa mchezo mmoja mmoja wakati Gulioni wana point 1 kwa michezo 2.

Ligi hiyo itaendelea tena kesho Jumatano kwa kupigwa mchezo mmoja katika Uwanja wa Amaan majira ya saa 10 za jioni kati ya Kwerekwe City dhidi ya Amaan Fresh.

Bingwa na Makamo Bingwa katika ligi hiyo watawakilisha Wilaya ya Mjini kwenda kucheza na Wilaya nyengine sita zikiwemo Magharibi “A”, Magharibi “B”, Kaskazini “A”, Kaskazini “B”, Kati na Wilaya ya Kusini kwa kucheza ligi ya Mabingwa wa Wilaya ambayo itakuwa na timu 14 huku timu 4 zikitafutwa kupanda Daraja la Pili Taifa Msimu ujao.

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE