MUANDISHI WA BOMBA FM APATA BONGE LA SHAVU

Suleiman Ussi Haji “Mido” ambae ni muandishi na mtayarishaji wa kipindi cha michezo cha SPORTS BOMBA cha Bomba FM amechaguliwa kuwa afisa Habari wa Kamati ya Soka Ufukweni visiwani Zanzibar.

Mara baada ya Chama cha Soka Visiwani Zanzibar kupata uanachama wa kudumu wa 55 wa Shirikisho la Soka Barani Afrika “CAF” wakaitaka Kamati ya soka la ufukweni kuunda uongozi mpya ambao rasmi kwasasa umewekwa hadharani.

Uongozi huo ambao unaongozwa na Ali Sharifu “Adolf” ambae ni Mwenyekiti, Katibu Fahad Khamis, mshika fedha Hassan Ali Mzee, mjumbe Ali Omar Abdallah huku Muhsin Ali “Kamara” na Mohd Rajab ni washauri wa kamati hiyo ambapo Afisa Habari ni Suleiman Ussi Haji “Mido” .

Tayari kamati hiyo imeshapata baraka zote kutoka ZFA taifa na imepania kuanza rasmi majukumu yake.

Comments

Popular posts from this blog

HUYU NDIYE MCHEZAJI MWENYE REKODI YA KUFUNGA MAGOLI MENGI KWENYE MECHI YA TAIFA DHIDI YA BOYS