RIKODI MUHIMU ZA TAIFA YA JANG’OMBE NA JANG’OMBE BOYS USO KWA USO KABLA MCHEZO WA LEO

Kikosi cha Taifa ya Jang'ombe


Timu ya Jang’ombe Boys inarikodi nzuri ya kumtesa Taifa ya Jang’ombe baada ya kukutana mara 6 ambapo Boys ameshinda mara 3 huku Taifa akishinda mara 2 na mchezo mmoja kwenda sare.

Wawili hao wote kutoka Mtaa mmoja wa Jang’ombe watakutana tena leo majira ya saa 2:00 za usiku katika Uwanja wa Amaan kwenye mchezo wa ligi kuu soka ya Zanzibar hatua ya 8 bora.

Kikosi cha Jang'ombe Boys

RIKODI USO KWA USO BOYS V/S TAIFA

WAMEKUTANA MARA 6 MPAKA SASA
Msimu wa mwaka 2012-2013
Ligi Daraja la Pili Wilaya ya Mjini Taifa 1-2 Boys.
Ligi ya Waamuzi dakika 90 Taifa 0-0 Boys, Penalti Taifa 4-5 Boys.

Novemba 19, 2016
Bonanza la Coconut FM Taifa 2-0 Boys.
Mabao yalifungwa na Mkongo Baraka Ushindi na Mkenya Mohd Said “Mess.

Disemba 10, 2016
Ligi kuu soka ya Zanzibar kanda ya Unguja Mzunguko wa kwanza Taifa 2-2 Boys.
Mabao ya Taifa siku hiyo alifunga Omar Yussuf Chande dakika 9 na Abdallah Mudhihir (Mido) dakika 60 wakati mabao ya Boys yote alifunga Khamis Mussa (Rais) dakika ya 45 na 53.

Disemba 30, 2016
Kombe la Mapinduzi 2017 Taifa 1-0 Boys
Bao pekee lililofungwa na Hassan Seif “Banda”.

April 25, 2017
Ligi kuu soka ya Zanzibar kanda ya Unguja mzunguko wa pili Taifa ya Jang’ombe 0-1 Jang’ombe Boys.

Bao pekee limefungwa na Khamis Mussa (Rais).

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE