TAIFA WAITAIFUTIA DAWA BOYS BAADA YA LEO KUFANYA MKUTANO MAALUM, HATUA YA 8 BORA WATAANZA KUKUTANA JUMAPILI HII DABI NYENGINE HIYO YA JAN’GOMBE


Wachezaji na Mashabiki wa Taif

Mashabiki, Wapenzi, Wachezaji na Viongozi wa timu ya Taifa ya Jang’ombe wamekutana kwa pamoja asubuhi ya leo kwa kujadili mambo mbali katika hatua ya 8 bora ambayo inatarajiwa kuanza wiki ijayo huku wakipania kutwaa ubingwa wa ligi kuu soka ya Zanzibar.

Mkutano huo umefanyika leo Jumapili Mei 7, 2017 kuanzia saa 4:00 za asubuhi katika Ukumbi wa SACCOS uliopo Meli nne mkabala na Shule ya Mbarali ambapo wamejadili mambo mengi ikiwa kujipanga katika hatua ya 8 bora ambapo mchezo wao wa kwanza Taifa watacheza na ndugu zao Jang’ombe Boys katika Uwanja wa Amaan saa 2:00 za usiku Jumapili ya Mei 14, 2017.

Katika Mkutano huo uliwapa fursa Wapenzi na Wachezaji kuchangia mawazo tofauti ili timu hiyo ifanye vizuri na kutimiza lengo lao la kubeba ubingwa wa Zanzibar.


“Lengo la Mkutano huu ni katika mpango wa kuzidi kuiboresha timu yetu tufanye vizuri katika hatua ya 8 bora na kubeba ubingwa wa Zanzibar”. Alisema Abdul kadir Gharib “Chabala” Meneja wa Taifa ya Jang’ombe.

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE