TAIFA WAMCHAGUA MWANASHERIA MAARUFU ZANZIBAR

Wakili msomi wa kujitegemea Omar Mmadi Mwarabu amechaguliwa kuwa Mwanasheria wa klabu ya Taifa ya Jang'ombe.

Akithibitisha taarifa hizo Katibu wa Taifa Mohammed Maulid "Edi Sada" amesema kutokana na soka la sasa linavyokwenda wamelazimika kumchagua Mwarabu kuwa Mwanasheria wao ambae ataongoza mambo yote ya kisheria yanayohusu klabu yao.

“Uongozi wa Taifa tumemteuwa Omar Mmadi kuwa mwanasheria wetu na atasimamia na kulinda haki zote za wachezaji, haki za timu na mambo yote ya kisheria kwa timu yetu ya Taifa”. Alisema Mohammed.

Kwa upande wake Mwanasheria huyo Omar Mmadi Mwarabu amepokea kwa furaha sana kuteuliwa kwenye timu hiyo kuwa Mwanasheria na anaimani kuwa haki zote za Taifa kwasasa hazitopotea tena baada ya uteuzi wake.


“Nimefurahi kuchaguliwa kuwa Mwanasheria, najua Uongozi wa Taifa wananijua kuwa mimi ni Taifa damu damu, nawaahidi haki zote za Taifa ntazilinda na kuzisimamia ipasavyo”. Alisema Mwarabu.

Mwanasheria huyo leo ametambulishwa mbele ya Uongozi,  Wachezaji na Mashabiki katika hafla maalum iliyofanyika mchana wa leo kwenye ukumbi wa Saccos Meli Nne Mbarali.
Omar Mmadi Mwarabu Mwanasheria wa Taifa

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE