TIMU YA KISANDU YATOKA SARE WAKIWA PUNGUFU WACHEZAJI 2, KESHO MECHI 7 KUPIGWA NYENGINE
Na: Fatma Suleiman, Zanzibar.
Timu ya Chuo cha Uandishi wa Habari Zanzibar “ZJMMC”
inayofundishwa na kocha Abubakar Khatib “Kisandu” jana ilitoka sare ya 1-1
dhidi ya Chuo cha Afya Mbweni katika Mashindano ya Vyuo Vikuu na Taasisi za
Elimu ya Juu Zanzibar “ZAHILFE CUP” uliopigwa majira ya saa 10 za jioni katika
Uwanja wa Amaan.
![]() |
Mchezo huo ni wa Kundi D ambapo ZJMMC walimaliza wakiwa
pungufu wachezaji wawili baada ya Walinzi wao kuonyeshwa kadi nyekundu Nassor
Cholo na Said Shaha katika dakika 54 ya mchezo na 67, mchezo ambao umesimamiwa na
Muamuzi mwenye beji ya FIFA Mgaza Ali Kinduli.
![]() |
Mashindano hayo yataendelea
tena kesho kwa kupigwa michezo tofauti katika viwanja tofauti.
Comments
Post a Comment