ZIMAMOTO YAKAMILISHA IDADI YA TIMU 8 ZILIZOFUZU 8 BORA

ZIMAMOTO YAKAMILISHA IDADI YA TIMU 8 ZILIZOFUZU 8 BORA

Timu ya Zimamoto imefanikiwa kutinga hatua ya 8 bora kwenye ligi kuu soka ya Zanzibar wakiwa na mchezo mmoja mkononi baada ya kupata ushindi mchana wa leo wa mabao 6-2 dhidi ya Chwaka Stars mchezo uliopigwa katika uwanja wa Amaan.

Mabao ya Zimamoto yamefungwa na Hassan haji dakika ya 1,48,65, Yussuf Ramadhan dakika ya 27, Idrisa Simai dakika ya 45 na Nyange Othman dakika ya 56.

Mabao ya Chwaka yamefungwa na 
Ali Bai dakika ya12 na
Abdul latif Mzee dakika ya 80.

Timu nyengine zilizofanikiwa kutinga hatua hiyo ni JKU, Jang’ombe Boys, Taifa ya Jang’ombe na Zimamoto
ambapo kwa upande wa Pemba ni Jamhuri, Mwenge, Kizimbani na Okapi zote kutoka mkoa wa kaskazini Pemba.

Hatua ya 8 bora ndio inayotowa Bingwa na Makamo Bingwa ambao watawakilisha Zanzibar katika Mashindano ya Kimataifa ya Klabu Bingwa na Kombe la Shirikisho Barani Afrika.

Hatua hiyo inatarajiwa kuanza punde tu itakapomalizika ligi zinazoendelea kwa Kanda zote za Pemba na Unguja ambazo zinatarajiwa kumalizika Mei 7, 2017.
Kikosi cha Zimamoto

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE