KAMA KAWAIDA YAO UNGUJA NA LEO MECHI YA 5 MFULULIZO WASHINDA, LAKINI YAHARIBU RIKODI YAKE YA KUTOTINGISHWA NYAVU ZAO, SASA WANA POINT 15 MABAO 15, JIONI WANACHEZA TENA MECHI NYENGINE LEO LEO

Kikosi cha Unguja
Leo timu ya soka ya Unguja imeendelea kucheza mchezo wake mwengine na kufanikiwa kushinda mabao 2-1 dhidi ya Iringa, mchezo uliopigwa saa 2 za asubuhi katika uwanja wa Chuo cha Ualimu Butimba Mkoani Mwanza kwenye mashindano ya UMISSETA.

Mabao ya Unguja leo yamefungwa na Iliyasa Suleiman na Mundhir Abdallah.

Ukiachia mchezo huo wa asubuhi pia Unguja leo jioni saa 10 watacheza mchezo wao wa mwisho wa kundi C dhidi ya timu ya Dar es salam ambao wao leo asubuhi hawajacheza wakati wenzao Unguja watacheza michezo 2 mfululizo kwa siku moja.

bado Unguja ndio kinara akiwa na alama 15, wakifukuzwa na Dar es salam wenye alama 13 wote wameshacheza michezo 5 na lakini timu zote hizo mbili zimeshakata tiketi ya kucheza hatua ya robo fainali.


Unguja wapo kundi “C” lenye jumla ya timu 7 ambapo wapo pamoja na Katavi, Kagera, Mara, Mbeya, Iringa na Dar es salam.


Michezo mitano ya awali Unguja waliifunga Katavi 4-0, wakaichapa Kagera 3-0, juzi wakaipiga Mara 5-0, jana waituguwa Mbeya 1-0, na leo wakaipiga Iringa 2-1, hivyo wameshafunga jumla ya mabao 15 katika michezo 5 waliyocheza wakati lango lao limeruhusu kufungwa bao moja tu.

Comments

  1. Nasema tena Zanzibar Vipaji vipo tatizo kuendelezwa FA na Walimu na wasimamizi wa timu tujiangalie sana nahisi tunajiona ni viongozi wa mpira kumbe ni wauwaji wa vipaji.

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE