NINJA WA YANGA APOKELEWA KISHUJAA NA TAIFA YA JANG’OMBE

Mlinzi mpya wa klabu ya Yanga aliyesajiliwa jana Abdallah Haji Shaibu "Ninja" amepokelewa kwa shangwe na mamia ya mashabiki wake punde tu alipowasili Visiwani Zanzibar mchana wa leo akitokea Jijini Dar es salam ambako alisaini mkataba wa miaka miwili kuitumikia klabu hiyo.

Mashabiki hao walianza kumpokea tangu Bandarini Malindi na kumpandisha gari aina ya Canter hadi nyumbani kwao Jang’ombe huku njiani wakimuimbia nyimbo na kupiga dufu kuashiria furaha ya mpendwa wao huyo kusajiliwa Yanga.

Rais wa Mashabiki wa Taifa ya Jang’ombe Ismail Ibrahim “Aili” aliongoza msafara huo ambao ulikuwa na furaha ya aina yake.

Ninja jana amesajiliwa Yanga akitokea timu ya Taifa ya Jang’ombe inayoshiriki ligi kuu soka ya Zanzibar.
Ninja akisaini jana mbele ya katibu wa Yanga Mkwasa

Comments

Popular posts from this blog

WACHEZAJI WA 5 WA ZANZIBAR HEROES WAMEITWA TIMU YA TAIFA YA TANZANIA TAIFA STARS KWAAJILI YA MICHEZO MIWILI YA KIMATAIFA YA KALENDA YA FIFA.

ZANZIBAR KARIBU WATAPATA UANACHAMA WA FIFA BAADA YA KUWA MWANACHAMA WA 55 WA CAF

JKU ACADEMY HAO WATANGULIA KWENDA ARUSHA KATIKA MASHINDANO YA ROLLING STONE